Home » » JENGENI UTAMADUNI WA KUWAPENDA NA KUWAHESHIMU WAGONJWA-MAKINDA

JENGENI UTAMADUNI WA KUWAPENDA NA KUWAHESHIMU WAGONJWA-MAKINDA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Madaktari Bingwa wakiendelea kumpa huduma mmoja wa wangonjwa wa macho katika hospitali ya Sokoine Lindi.
Baadhi ya vifaa tiba na dawa zilizotumika katika zoezi hilo vikikabidhiwa kwa mkuu wa mkoa wa Lindi Bwana Godfrey Zambi.
 Daktari Bingwa wa watoto Martha Mkonyi akimuhudumia mmoja wa watoto waliokuja kupata huduma.

MWENYEKITI wa Bodi  ya Wakurugenzi wa Mfuko  wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Spika Mstaafu  Anne Makinda amewahimiza watoa huduma katika vituo vya matibabu kujenga utamaduni wa kuwapenda na kuwaheshimu wagonjwa ili kuwapa faraja na huduma bora wanapokwenda kupata matibabu katika vituo vyao.

Akizunguza wakati wa uzinduzi wa huduma za madaktari bingwa katika mikoa ya Mtwara na Lindi, Mama Makinda amesema wagonjwa wengi hususan wanawake wajawazito wanaogopa kwenda kupata huduma za mazitbabu katika vituo hivyo kutokana na mapokezi mabaya wanayopata hivyo wanaamua kwenda kwa wakunga wa jadi au kujifungulia majumbani ambako hakuna mazingira salama.

Amesisitiza kuwa wahudumu wa vituo vya matibabu wanawajibika kuwa na lugha nzuri na huruma kwa wagonjwa kwani kazi wanayofanya inaweza kuwa na mafanikio au madhara makubwa kwa afya za watu wanapwahudumia.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bwana Bernald Konga amesema Mfuko huo umepania kufikisha huduma bora kwa kila mtanzania hivyo hatua ya kupeleka madaktari bingwa katika mikoa yenye mahitaji makubwa ya huduma hiyo ni hatua mojawapo ya kusogeza huduma karibu na watanzania wengi.

Amesema kuanzia mwaka 2013 hadi sasa Mfuko umeshapeleka madaktari bingwa katika mikoa 17 ambapo mikoa minne imepata huduma hizo mara mbili. Mikoa hiyo ni pamoja na Kigoma, Rukwa, Lindi na Mtwara. 

Ameongeza kuwa katika kipindi cha miaka minne cha utekelezaji wa mpango huo katika mikoa ya pembezoni zaidi ya wananchi Elfu Kumi na Tisa wamehudumiwa na madaktari bingwa ambapo zaidi ya Mia saba wamefanyiwa upasuaji wa kibingwa.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa