Home » » WAJUMBE MKUTANO MKUU WA 45 CHAMA CHA WAUGUZI TANZANIA (TANNA) SAFARINI LINDI

WAJUMBE MKUTANO MKUU WA 45 CHAMA CHA WAUGUZI TANZANIA (TANNA) SAFARINI LINDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.



 Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wauguzi Tanzania  (TANNA)  kutoka sehemu mbalimbali wakiungana na wajumbe wenzao pamoja na viongozi wa Tanna Mkoa wa Lindi jana katika kufanya maandalizi ya Mkutano Mkutano Mkuu  wa 45 unao tarajiwa kufanyika Oktoba 4-6 Kitaifa  ambapo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Mh. Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa.( PICHA ZOTE NA KHAMISI MUSSA)

 Mwenyekiti wa Chama Cha Wauguzi Tanzania (TANNA) Mkoa wa Lindi, Patrick Achimpota (kulia) mwenyeshati la kitenge akisalimiana na mjumbe wa Kamati kuu ya Chama hicho kutoka Arusha, Hosea Naman mara alipofika Mkoani humo kwa niaba ya Mkutano Mkuu wa Chama hicho.


 Wajumbe wa Chama Cha Wauguzi (TANNA) wakiwa katika safari kuelekea Mkoa wa Lindi katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho  unao tarajiwa kufanyika Oktoba 4-6 Kitaifa ambapo unatarajiwa kufunguliwa na Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa.



 Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Lindi, Damasiana Msala (kulia)  akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Wauguzi (TANNA) mara walipowasili katika mkoa huo jana
 Makamu wa Rais wa Chama hicho, Ibrahim Mgoo (wa katikati) akisalimia wajumbe mara baada ya kuwasili katika Mkoa huo jana, kulia ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Mkoa Lindi, Damasiana Msala na kushoto ni Katibu Mkuu wa Chama hicho, Sebastian Luziga. 

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa