Home » » SHULE ZA UDONGO ZAMKERA RC.

SHULE ZA UDONGO ZAMKERA RC.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
ELIMU bora haiwezi kupatikana mkoani Lindi kama hakutakuwapo mikakati maalumu kuondoa tatizo la shule zilizojengwa kwa udongo, miti na ukosefu wa vyoo katika shule za msingi zenye zaidi ya miaka 30, imeelezwa.
Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Jordan Rugimbana ameyasema hayo jana wakati alipozungumza na vyombo vya habari ofisini kwake na kueleza kuwa kuna shule za msingi zina matatizo mbalimbali ikiwemo wanafunzi wanasoma chini miti, vyumba vyao vya madarasa bado vya udongo na ukosefu wa vyoo.
Uongozi wa mkoa sasa unatakiwa kuhakikisha tatizo hilo linawekewa mikakati ili kuondoa tatizo hilo la muda mrefu nalo ni moja ya chanzo cha kushuka kwa elimu kutokana mazingira yake siyo mazuri ya kusomea.
“Mamlaka zote zinatakiwa kuhakikisha zinafanya kazi zake kwa ushirikiano wa kutosha kuweza kuondoa kero hizo kila moja kuanzia ngazi ya Mkoa, Halmashauri za Wilaya na Manispaa.
Haiwezekani wanafunzi wasome chini ya miti, udongo au nyumba ya mwalimu ya udongo halafu useme kuwa inatakiwa kuwapo elimu bora kwa wanafunzi itakuwa ni ndoto,” alisema.
Aidha, aliongeza kuwa tatizo hilo linaendana na la afya kwa vifo vya mama na mtoto, navyo vinaleta athari mbaya kwa mkoa kutoka kituo cha tiba kwenda kijijini ni hatua. Rugimbana alisema vifo hivyo vinatokea njiani kwani mama akishafikia wakati wa kujifungua au mtoto anahitajika kwenda hospitalini au kituo cha afya, hapo kuna umbali kwa bahati mbaya anafariki.
Alisema ni wajibu wa mamlaka husika kuona tatizo hilo na kuchukua hatua za kuliondoa kutokana na kupunguza nguvu kazi kwani unapompoteza mama au mtoto unapoteza moja ya fursa za uchumi.
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa