Home » » MVUA YAATHIRI KAYA 200

MVUA YAATHIRI KAYA 200

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KAYA 200 kutoka kitongoji cha Namadingula katika Kata ya Rasibura mjini Lindi wilayani humo wameharibiwa makazi, mashamba ya mazao ya mahindi na ufuta kutokana mvua zinazoendelea kunyesha mjini hapa.
Diwani wa Kata ya Rasbura, Abdallah Kikwei aliyasema hayo jana wakati akizungumza na gazeti hili ofisini kwake mjini hapa, na kueleza kuwa wakazi hao walikumbwa na kadhia hiyo baada ya kunyesha mvua kubwa iliyoambatana na upepo mkali usiku wa juzi kuamkia jana.
Hali hiyo inaendana na ya ukosefu wa vyakula, hivyo itasababisha kuwapo njaa kwa wakazi hao kutokana vyakula vyao ambavyo vilihifadhiwa ndani kwa ajili ya matumizi yao kila siku vilichukuliwa na maji.
Alifafanua uongozi wa kata uliamua kwenda kufanya ukaguzi na kubaini tatizo hilo, na watapeleka taarifa kwa uongozi wa wilaya kuwasaidia wakazi hao kwa makazi na mahitaji mengine.
Hata hivyo, alisema mpaka sasa yeye atapeleka tani 200 za mahindi kwa ajili ya kuwapatia mbegu na tani 100 kwa zao la ufuta ili msimu unaokuja kuendelea kulima mazao hayo. Kikwei alisema mvua hiyo iliathiri wakazi wa Mitwero Stendi kutokana na baadhi ya nyumba kujengwa karibu na njia ya maji yanayotoka katika mto na nyumba zao ziliharibika. Aliongeza kuwa nyumba kadhaa za maeneo hayo ziliingiliwa na maji hayo hususan ya mto Mitwero ambayo yanapofurika huwa yanapita kwenda baharini
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa