Home » » VYAMA VYA USHIRIKA VYADAIWA SH MIL 700.

VYAMA VYA USHIRIKA VYADAIWA SH MIL 700.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
VYAMA sita vya msingi vya ushirika wilayani Liwale mkoani hapa vinadaiwa na wakulima Sh mil 700 kutokana na kukusanya korosho bila kuwalipa katika msimu wa 2015/2016.
Mwenyekiti wa kamati ya muda inayosimamia vyama vya msingi vya ushirika katika wilaya za Ruangwa, Nachingwea na Liwale (RUNALI), Azizi Liega, aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na gazeti hili mjini hapa.
Alisema, madai hayo ni kwa ajili ya mauzo ya tani 350 kati ya tani 19,000 za korosho zilizokusanywa na vyama hivyo na kupelekwa katika maghala kwa mauzo.
Mwenyekiti huyo wa kamati ya muda alifafanua kuwa, deni hilo kwa vyama hivyo linatokana na kuuza korosho kwenye mnada mwezi uliopita na kupatikana wanunuzi, lakini hawakuweza kutoa fedha kwa wakati unaotakiwa.
Alisema, hali hiyo ilichelewesha malipo kwa wakulima hao na vyama kubaki na deni, lakini bado korosho zipo katika maghala mpaka hapo wanunuzi hao watakapofika na kulipa.
Alisema kampuni zilizoahidi kulipa zitafika Ijumaa wiki hii na kulipa deni hilo ili kuzichukuwa korosho hizo tayari kuzisafirisha ndani na nje ya nchi.
 CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa