Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
VYAMA sita vya msingi vya ushirika wilayani Liwale mkoani hapa 
vinadaiwa na wakulima Sh mil 700 kutokana na kukusanya korosho bila 
kuwalipa katika msimu wa 2015/2016.
Mwenyekiti wa kamati ya muda inayosimamia vyama vya msingi vya 
ushirika katika wilaya za Ruangwa, Nachingwea na Liwale (RUNALI), Azizi 
Liega, aliyasema hayo jana wakati alipokuwa akizungumza na gazeti hili 
mjini hapa.
Alisema, madai hayo ni kwa ajili ya mauzo ya tani 350 kati ya tani 
19,000 za korosho zilizokusanywa na vyama hivyo na kupelekwa katika 
maghala kwa mauzo.
Mwenyekiti huyo wa kamati ya muda alifafanua kuwa, deni hilo kwa 
vyama hivyo linatokana na kuuza korosho kwenye mnada mwezi uliopita na 
kupatikana wanunuzi, lakini hawakuweza kutoa fedha kwa wakati 
unaotakiwa.
Alisema, hali hiyo ilichelewesha malipo kwa wakulima hao na vyama 
kubaki na deni, lakini bado korosho zipo katika maghala mpaka hapo 
wanunuzi hao watakapofika na kulipa.
Alisema kampuni zilizoahidi kulipa zitafika Ijumaa wiki hii na kulipa
 deni hilo ili kuzichukuwa korosho hizo tayari kuzisafirisha ndani na 
nje ya nchi.
 CHANZO : HABARI LEO.
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment