Home » » WAKULIMA LIWALE KUNUFAIKA NA MBEGU ZA ALIZETI, UFUTA

WAKULIMA LIWALE KUNUFAIKA NA MBEGU ZA ALIZETI, UFUTA

Chama cha Kuuza na Kununua Mazao cha Umoja, kilichopo wilayani Liwale, Mkoa wa Lindi kimeanza kutekeleza mradi wa kugawa mbegu za alizeti na ufuta kwa wakulima zaidi ya 700 zenye thamani ya Sh6 milioni.
Mwenyekiti wa chama hicho, Hassan Mpako alisema hayo jana katika uzinduzi wa mpango huo.
Alisema lengo lao ni kuwawezesha wakulima kulitumia zao hilo mbadala wa korosho na ufata.
Mpako alisema wakulima watafaidika kutokana na kuwezeshwa kiteknolojia, ikiwamo kupewa mashine na utaalamu wa utayarishaji wa mafuta ya alizeti.
Alisema kwa awamu ya kwanza, mradi huo utatekelezwa katika kata za majaribio za Nangando, Liwale na Likongowele.
Alisema hali hiyo itasaidia kubaini na kupunguza vikwazo wanavyopata wakulima wa korosho ili waone namna ya kutumia fursa nyingine badala ya kuendelea kuilaumu Serikali kwa kukosa soko la korosho.
Katibu Tawala Wilaya Liwale, Jocob Nyamanga aliwataka wakulima hao kutumia fursa hiyo kuongeza uzalishaji ili kujipatia mapato ya ziada.
“Mpango huu ni mzuri, hivyo ni vyema vyama vyote vya ushirika vikaiga utaratibu Chama cha Umoja wa kuwapatia mbegu za alizeti wanachama wao,” alisema Nyamanga.
 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa