Home » » WAKAZI WA KIJIJI CHA KITWAVI WALALAMIKIA KUAPISHWA MWENYEKITI WA CCMAMBAYE HAJASHINDA.

WAKAZI WA KIJIJI CHA KITWAVI WALALAMIKIA KUAPISHWA MWENYEKITI WA CCMAMBAYE HAJASHINDA.

Wakazi wa kijiji cha kitwavi kilichopo katika kata ya  matimba halmashauri ya lindi vijijini wameilalamikia  serikali kufuatia kuapishwa   mgombea  wa nafasi ya uenyekiti wa kijiji hicho kwa tiketi ya CCM kuwa mshindi katika uchaguzi wa serikali za mitaa   kwa madai kuwa mshindi halali alikuwa mgombea  kutoka chama cha wananchi CUF.
Wakizungumza na ITV wakazi wa kijiji hicho wamesema   hawatomtambua wala kumpa ushirikiano mgombea wa chama cha mapinduzi endapo ataapishwa kuwa mwenyekiti, kwa kuwa awali msimamizi wa uchaguzi katika kijiji hicho alishamtangaza mgombea wa CUF kuwa mwenyekiti wa kijiji hicho ambapo pia wanakijiji hao wameleeza kushangazwa na kitendo cha mgombea wa CCM kuhudhuria shughuli ya kuapishwa ikiwa mshindi alikuwa mgombea wa CUF na kwamba maelelezo ya msimamizi wa  uchaguzi kijijini hapo hayana ukweli wowote.
 
Msimamamizi wa uchaguzi katika kijiji hicho ambaye amekiri kumtangaza mgombea wa chama cha wananchi CUF kuwa mshindi na kuongeza kuwa alilazimika kufanya hivyo kufuatia shinikizo lililotolewa na baadhi ya wanachama wa chama cha wananchi CUF  waliokuwa wamezingira wakiwa na silaha za jadi jengo ambamo zoezi la uhesabuji kura za vitongoji vyote vya kijiji hicho likiwa linaendelea  ambapo pia amekanusha madai  ya kuwa mgombea wa CUF ndiye aliyeibuka mshindi  na kwamba mgombea wa chama cha mapinduzi ccm ndiye mshindi  katika uchaguzi huo.
 
ITV ikamtafuta mkurugenzi wa halmashauri ya lindi vijijiini na kuzungumza nae ambapo amesema kuwa, alipokea taarifa hizo na kwamba taarifa ya kuwepo vurugu zilizopelekea kupotoshwa kwa taarifa za matokeo katika kijiiji hicho licha ya kuwepo kwa ulinzi wa mgambo zipo katika ngazi ya polisi wilaya, ambapo ameongeza kuwa hajapokea barua yoyote ya kuitwa mahakamani licha ya walalamikaji kupewa muda wa kuwasilisha malalamiko yao katika vyombo vya sheria.
 
Kwa matokeo ya awali yaliyotangazwa na masimamizi wa uchaguzi kijijini hapo yalionyesha  kuwa chama cha wananchi CUF katika nafasi ya mwenyekiti ndicho kilichoibuka mshindi kwa kura 102 dhidi ya mgombea wa CCM aliyepata kura 99, jambo linaloibua hali ya sintofahamu endapo mgombea wa ccm ataapishwa kuwa mwenyekiti wa kijiji hicho.
Chanzo:ITV Tanzania
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa