Wakazi
 wa kijiji cha kitwavi kilichopo katika kata ya  matimba halmashauri ya 
lindi vijijini wameilalamikia  serikali kufuatia kuapishwa   mgombea  wa
 nafasi ya uenyekiti wa kijiji hicho kwa tiketi ya CCM kuwa mshindi 
katika uchaguzi wa serikali za mitaa   kwa madai kuwa mshindi halali 
alikuwa mgombea  kutoka chama cha wananchi CUF.
Wakizungumza na ITV wakazi wa kijiji hicho wamesema   hawatomtambua
 wala kumpa ushirikiano mgombea wa chama cha mapinduzi endapo ataapishwa
 kuwa mwenyekiti, kwa kuwa awali msimamizi wa uchaguzi katika kijiji 
hicho alishamtangaza mgombea wa CUF kuwa mwenyekiti wa kijiji hicho 
ambapo pia wanakijiji hao wameleeza kushangazwa na kitendo cha mgombea 
wa CCM kuhudhuria shughuli ya kuapishwa ikiwa mshindi alikuwa mgombea wa
 CUF na kwamba maelelezo ya msimamizi wa  uchaguzi kijijini hapo hayana 
ukweli wowote.
Msimamamizi wa uchaguzi katika kijiji hicho ambaye amekiri 
kumtangaza mgombea wa chama cha wananchi CUF kuwa mshindi na kuongeza 
kuwa alilazimika kufanya hivyo kufuatia shinikizo lililotolewa na baadhi
 ya wanachama wa chama cha wananchi CUF  waliokuwa wamezingira wakiwa na
 silaha za jadi jengo ambamo zoezi la uhesabuji kura za vitongoji vyote 
vya kijiji hicho likiwa linaendelea  ambapo pia amekanusha madai  ya 
kuwa mgombea wa CUF ndiye aliyeibuka mshindi  na kwamba mgombea wa chama
 cha mapinduzi ccm ndiye mshindi  katika uchaguzi huo.
ITV ikamtafuta mkurugenzi wa halmashauri ya lindi vijijiini na 
kuzungumza nae ambapo amesema kuwa, alipokea taarifa hizo na kwamba 
taarifa ya kuwepo vurugu zilizopelekea kupotoshwa kwa taarifa za matokeo
 katika kijiiji hicho licha ya kuwepo kwa ulinzi wa mgambo zipo katika 
ngazi ya polisi wilaya, ambapo ameongeza kuwa hajapokea barua yoyote ya 
kuitwa mahakamani licha ya walalamikaji kupewa muda wa kuwasilisha 
malalamiko yao katika vyombo vya sheria.
Kwa matokeo ya awali yaliyotangazwa na masimamizi wa uchaguzi 
kijijini hapo yalionyesha  kuwa chama cha wananchi CUF katika nafasi ya 
mwenyekiti ndicho kilichoibuka mshindi kwa kura 102 dhidi ya mgombea wa 
CCM aliyepata kura 99, jambo linaloibua hali ya sintofahamu endapo 
mgombea wa ccm ataapishwa kuwa mwenyekiti wa kijiji hicho.
Chanzo:ITV Tanzania 
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment