Home » » MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA KATA ZA MIKUMBI,NDARO NA MBANJA HUKO LINDI

MAMA SALMA KIKWETE ATEMBELEA KATA ZA MIKUMBI,NDARO NA MBANJA HUKO LINDI


Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokewa na Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi Ndugu Regina Chonjo mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Lindi tarehe 11.12.2014.
NGAPI???"Mbiliii;-Hivi ndivyo mke wa rais Mama Salma Kikwete, alipowauliza wana Ndaro kuhusu muundo gani wa serikali unaokubalika nchini, na kujibiwa serikali mbili.Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akishirikiana na viongozi wa CCM wa Kata ya Ndaro kuunga mkono muundo wa serikali mbili unaopendekezwa na Rasimu ya Katiba, wakati akiwa kwenye kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa huko Lindi leo Alhamisi Desemba 11, 2014. Uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika kote nchini Desemba 14, 2014
Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akishirikiana na viongozi wa CCM wa Kata ya Ndaro kuunga mkono muundo wa serikali mbili unaopendekezwa na Rasimu ya Katiba, wakati akiwa kwenye kampeni za uchaguzi wa serikali za mitaa huko Lindi leo Alhamisi Desemba 11, 2014. Uchaguzi wa serikali za mitaa utafanyika kote nchini Desemba 14, 2014
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akisalimiana na viongozi wa CCM Kata ya Mikumbi iliyoko Mjini Lindi wakati alipowasili kwenye eneo hilo kwa ajili ya kufanya mkutano wa ndani na viongozi hao tarehe 11.12.2014. Anayemtambulisha kwa wajumbe hao ni Mwenyekiti wa CCM wa Kata ya Mikumbi Bwana Bakari Seif Mikojo.
Mjumbe wa NEC Taifa ya CCM anayewakilisha Wilaya ya Lindi Mjini na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwatambulisha na kuwaombea kura wagombea uenyekiti wa serikali za mitaa wa Kata ya Ndaro kwa wajumbe wa mkutano. Mama Salma yuko Wilayani Lindi Mjini kuhamasisha wananchi kukipigia kura Chama Cha Mapinduzi katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 14.12.2014.
Picha na John Lukuwi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa