Mjumbe
wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Mke wa Rais Mama
Salma Kikwete akizungumza katika kikao cha ndani na wajumbe wa Tawi la
Nanyanje lililopo katika Kata ya Chikonji katika wilaya ya Lindi Mjini .
Mjumbe
wa NEC Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwapungia
wananchi wa Kata ya Chikonji wakati alipofika kwenye Makao Makuu ya Kata
hiyo kwa ajili ya mkutano wa kampeni kwa ajili ya uchaguzi wa serikali
za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini
Mamia
ya wananchi waliofurika katika mkutano wa kampeni ulifanyika katika
Kata ya Chikonji iliyoko katika Wilaya ya Lindi Mjini na kuhutubiwa na
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Mama Salma Kikwete tarehe
12.12.2014.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akijiandaa kupokea kadi kutoka kwa Ndugu Abdallah Mohammed Kilimbalimba aliyekuwa mwanachama wa Chama Cha Wananchi (CUF) ambaye aliamua kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wakati wa mkutano wa kampeni huko Chikonji katika Wilaya ya Lindi Mjini
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayewakilisha Wilaya ya Lindi Mjini na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwahutubia mamia ya wananchi wa Kata ya Chikonji kwenye mkutano wa kampeni ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika nchini tarehe 14.12.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akimchukua mtoto Subira kutoka kwa mama yake ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja wakati wa mkutano wa kampeni huko Chikonji taqrehe 12.12.2014.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akiwasili kwenye Tawi la Makonde lililoko kwenye Kata ya Mingoyo katika Wilaya ya Lindi Mjini huku akipokewa kwa shangwe na vifijo kwa ajili ya mkutano wa kampeni tawini hapo
Baadhi ya akina mama wakishangilia kwa hisia kubwa wakati Mama Salma Kikwete alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni katika Kata ya Mingoyo uliofanyika katika Tawi la Makonde
Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Taifa Mama Salma Kikwete akihutubia mkutano wa kampeni katika Tawi la Makonde lililoko katika kata ya Mingoyo
Picha na John Lukuwi
***************
Na Anna Nkinda – Maelezo, Lindi
Wakazi wa wilaya ya Lindi mjini wametakiwa kuhakikisha watoto wao
wanakwenda shule na kusoma kwa bidii kwani Serikali ya Chama cha
Mapinduzi (CCM) imejenga shule za kutosha katika kata zote za wilaya
hiyo.
Mwito
huo umetolewa jana na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM
kupitia wilaya ya Lindi mjini Mama Salma Kikwete wakati akiongea kwa
nyakati tofauti na wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni ya uchaguzi
wa Wenyeviti na Wajumbe wa Serikali za mitaa uliofanyika katika Kata za
Chikonji na Mingoyo.
Mama
Kikwete ambaye ni Mke wa Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alisema wakati
ujenzi wa shule hizo unaanza vyama vya upinzani walizidharau na
waliziita za yeboyebu kwa lengo la kuwakatisha tamaa lakini Serikali ya
CCM kwa kushirikiana na wananchi hawakukata tamaa na kuendelea na
ujenzi.
“Zamani
wanafunzi waliokuwa wanajiunga na elimu ya Sekondari walikuwa wachache
baada ya kukamilika kwa ujenzi wa shule hizi hivi sasa kila mwanafunzi
anayefaulu mtihani wa darasa la saba anajiunga na elimu ya Sekondari
haya ndiyo maendeleo yaliyoletwa na CCM”.
Ili
uweze kuendelea ni lazima ukutane na changamoto nasi katika shule hizi
tulikutana na changamoto za walimu na maabara, vyuo mbalimbali nchini
viliweza kutoa walimu wengi na kupunguza tatizo la walimu wa masomo ya
sanaa na miaka michache ijayo watapatikana walimu wa kutosha wa masomo
ya sayansi”, alisema Mama Kikwete.
Aliendelea
kusema wakati wa ujenzi wa shule za Sekondari za Kata kulisahaulika
ujenzi wa maabara kwa ajili ya masomo ya sayansi, hivi sasa Serikali
kwa kushirikiana na wananchi wanamalizia kazi ya ujenzi wa maabara
katika shule hizo na hivyo kuwafanya watoto kusoma masomo ya sayansi
kwa fasaha zaidi.
MNEC
huyo pia aliwataka wananchi hao kuchagua viongozi wanaofaa kwani
uchaguzi ni kwa ajili ya kutengeneza maisha yao kwa kipindi cha miaka
mitano hivyo basi wasiweke rehani maisha yao kwa kufuata mkumbo na
kuchagua viongozi wasiofaa.
Kwa
upande wake Katibu wa CCM mkoa wa Lindi Adelina Gefi alisema katika
uchaguzi wa Serikali za mitaa, vijiji na vitongoji chama hicho kitapata
ushindi wa kishindo kwani hadi hivi sasa ndani ya mkoa huo wagombea
katika vitongoji 600, vijiji 80 na mitaa saba wamepita bila kupingwa.
Gefi
alisema CCM inaleta maendeleo na upinzani unachelewesha hivyo basi siku
ya uchaguzi ikifika wananchi wajitokeze kwa wingi na kuwachagua
wagombea wa chama hicho ili wawaletee maendeleo.
Katika
mkutano wa hadhara uliofanyika kata ya Chikonji mwanachama mmoja
aliyejulikana kwa jina la Abdallah Mohammed Kilimbalimba kutoka Chama
cha Wananchi (CUF) alijiunga na Chama Cha Mapinduzi.
Mama
Kikwete yupo wilayani humo kwa ajili ya kushiriki kwenye kampeni na
kuwanadi wagombea wa chama hicho wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi
katika uchaguzi wa viongozi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji
unaotarajiwa kufanyika kesho nchini.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment