Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
raia na kusababisha vifo vya watu watatu katika Kijiji cha Mnolela barabara kuu ya Mtwara Dar es Salaam.
Kifaru hicho chenye namba za usajili 018 mali ya JWTZ kikosi Namba 
83, iliyokuwa inaendeshwa na askari wa jeshi hilo, Shadhil Nandonde, 
ikitokea Mtwara kwenda Nachingwea.
Ajali hiyo ilitokea majira saa 11:30 alfajiri na kusababisha vifo vya
 watu wawili akiwemo askari Namba Mt 10728 Private Pascal Komba na Somoe
 Kamteule (75), mkazi wa Mnolela ambaye alikuwepo ndani ya nyumba moja 
kati ya zilizogongwa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Lindi, Renatha Mzinga, 
majeruhi wa ajali hiyo ni MT. 10744 Private Simon Edward, MT. 106842, 
Private Feruz Haji, MT. 1077263 Private Omary Makao, MT. 99018 Private 
Mbaruk Duch, MT. 107442  Private Simon Masele na MT. 107218 Private 
Ndekenya.
Kwa upande wake, Mganga Mkuu Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya 
Ligula, Dk. Lobikieli Kisambu, alithibitisha kwa njia ya simu kuwa 
alipokea maiti mbili na pamoja na mejeruhi sita.
Kwa mujibu wa Dk. Kisambu, kati ya majeruhi hao waliyopokelewa 
hospitalini hapo, mmoja amepelekwa hospitali ya Nyangao kutokana na hali
 yake kuwa si ya kuliridhisha na mmoja wao amefariki dunia akiwa 
anapatiwa matibabu na kufanya waliofariki kufikia watatu.
 Chanzo; Tanzania Daima 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment