Home » » UBABE: POLISI WAVAMIWA LINDI, MTUHUMIWA AUAWA

UBABE: POLISI WAVAMIWA LINDI, MTUHUMIWA AUAWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Kundi la vijana wasiofahamika kutoka mjini Liwale, mkoani Lindi, wamevamia Kituo cha Polisi Lionja na kuwazidi nguvu askari, kabla ya kumtorosha mtuhumiwa wa mauaji na kisha kumuua na mwili wake kuuchoma moto.
Aliyeuawa ametambulika kwa jina la Issa Mfaume (31), mkazi wa Likongowele aliyekuwa akishikiliwa kituoni hapo kwa tuhuma za mauaji ya Zalali Lunje (27) kwa kumchoma kisu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, Rainata Mzinga alisema tukio hilo lilitokea jana saa nne asubuhi, karibu na Kituo cha Mabasi cha Liwale.
Baadhi ya mashuhuda bila kutaka kutaja majina yao, waliliambia gazeti hili kuwa, vijana hao wakiwa na pikipiki walikwenda kituoni hapo na kuwatisha polisi kabla ya kumtorosha mtuhumiwa huyo wa mauaji.
Baada ya kufanikiwa kumtorosha mtuhumiwa aliyedaiwa kufanya mauaji mwishoni mwa wiki iliyopita, walimpeleka hadi eneo analotuhumiwa kufanya mauaji na kisha kuanza kumpa kichapo.
“Niliona kundi la vijana wakimpiga sehemu mbalimbali mwilini, aliishiwa nguvu na baadaye walimchoma moto hadi mwili wake kuteketea kabisa,” alisema shuhuda ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini.
Kamanda Mzinga alisema jeshi lake linawasaka wahusika wa mauaji na kisha kuwafikisha mahakamani kujibu tuhuma za kujichukulia sheria mkononi.
Amewataka wananchi kuepuka utamaduni wa kujichukulia sheria mikononi. “Sheria zipo, lazima zifuatwe na watakaokwenda kinyume wanatafuta matatizo,” alionya Mzinga.
Chaonzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa