Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tabora, umeikabidhi
Hospitali ya Rufaa Kitete msaada wa shuka 150 zenye thamani ya sh
milioni 3.5.
Akikabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, Balozi Ali Mchumo, alisema kuwa wataendelea kutoa msaada kulingana na
mahitaji ili kukabiliana na changamoto katika Hospitali ya Rufaa Kitete.
mahitaji ili kukabiliana na changamoto katika Hospitali ya Rufaa Kitete.
Mchumo alisema mfuko utaendelea kufanya hivyo kwani wao wana wajibu
wa kutoa misaada kwa ajili ya kuwawezesha wagonjwa kupata huduma nzuri.
Alisema kuwa shuka hizo zitapunguza adha ya wagonjwa kutumia kanga na vitenge kwa ajili ya kujifunika.
Akikabidhi msaada huo kwa Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk.
Dennis Kitapondya, Mchumo alisema kama mfuko wamejipanga kuendelea
kusaidiana na hospitali na vituo vya afya ili kukabiliana na changamoto
zinazowakabili.
Kuhusu uchakavu wa majengo na upungufu wa miundombinu, Mchumo
aliutaka uongozi wa hospitali hiyo kukopa kutoka katika mfuko huo kwani
hivi sasa wanakopesha vifaa mbalimbali, vikiwemo vipimo na vile vya
ukarabati ili kuweza kutoa huduma nzuri.
Awali Dk. Kitapondya akitoa taarifa fupi kwa mwenyekiti wa Bodi ya
NHIF, alisema wanakabiliwa na upungufu wa miundombinu ambayo imekuwa
ikisababisha msongamano na kusababisha wagonjwa kulala wawili katika
kitanda kimoja.
Pia aliongeza kuwa wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi, hasa
madaktari, na kwamba uongozi wa mkoa kwa jitihada zake uliweza
kuipatia hospitali hiyo madaktari 12 mwaka jana ambao hata hivyo
alisema hawatoshelezi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyimvua, aliishukuru NHIF
kwa msaada huo akisema kuwa hospitali hiyo ina vitanda 350 na shuka
zilizokuwepo ni 150 tu.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment