Home » » NHIF YAKABIDHI SHUKA ZA MIL.3.5/-

NHIF YAKABIDHI SHUKA ZA MIL.3.5/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) mkoani Tabora, umeikabidhi Hospitali ya Rufaa Kitete msaada wa shuka 150 zenye thamani ya sh milioni 3.5.
Akikabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, Balozi Ali Mchumo, alisema kuwa wataendelea kutoa msaada kulingana na
mahitaji ili kukabiliana na changamoto katika Hospitali ya Rufaa Kitete.
Mchumo alisema mfuko utaendelea kufanya hivyo kwani wao wana wajibu wa kutoa misaada kwa ajili ya kuwawezesha wagonjwa kupata huduma nzuri.
Alisema kuwa shuka hizo zitapunguza adha ya wagonjwa kutumia kanga na vitenge kwa ajili ya kujifunika.
Akikabidhi msaada huo kwa Mganga Mfawidhi wa hospitali hiyo, Dk. Dennis Kitapondya, Mchumo alisema kama mfuko wamejipanga kuendelea kusaidiana na hospitali na vituo vya afya ili kukabiliana na changamoto zinazowakabili.
Kuhusu uchakavu wa majengo na upungufu wa miundombinu, Mchumo aliutaka uongozi wa hospitali hiyo kukopa kutoka katika mfuko huo kwani hivi sasa wanakopesha vifaa mbalimbali, vikiwemo vipimo na vile vya ukarabati ili kuweza kutoa huduma nzuri.
Awali Dk. Kitapondya akitoa taarifa fupi kwa mwenyekiti wa Bodi ya NHIF, alisema wanakabiliwa na upungufu wa miundombinu ambayo imekuwa ikisababisha msongamano na kusababisha wagonjwa kulala wawili katika kitanda kimoja.
Pia aliongeza kuwa wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa watumishi, hasa madaktari, na kwamba uongozi wa mkoa kwa jitihada zake uliweza kuipatia hospitali hiyo madaktari 12 mwaka jana ambao hata hivyo alisema hawatoshelezi.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora, Kudra Mwinyimvua, aliishukuru NHIF kwa msaada huo akisema kuwa hospitali hiyo ina vitanda 350 na shuka zilizokuwepo ni 150 tu.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa