Home » » WAZAZI WAIBARIKI LSA ROLLINGSTONE 2014

WAZAZI WAIBARIKI LSA ROLLINGSTONE 2014

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZAZI na walezi wa wachezaji wa timu ya Lindi Soccer Academy (LSA), ya mjini hapa, wamebariki ushiriki wa kikosi hicho katika michuano ya mwaka huu ya vijana ya Rollingstone kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati chini ya mwamvuli wa East and Central African Youth Football Academies Association (ECAYFA).
LSA imealikwa kushiriki michuano hiyo ya vijana chini ya miaka 20 na 15 itakayofanyika kuanzia Julai 5- 14 kwenye viwanja vya Karume Ilala na Azam Complex, Chamazi jijini Dar es Salaam.
Wazazi hao walikubaliana kwa kauli moja katika mkutano uliofanyika ukumbi wa Double M Hotel, kuiwezesha LSA kushiriki michuano hiyo, ambapo waliafiki kuchangia gharama mbalimbali ikiwamo nauli, malazi na chakula, huduma ambazo timu za Tanzania zinapaswa kujigharamia zenyewe wakati wa mashindano.
Watu 50 wakiwamo wachezaji, viongozi na wazazi, walishiriki mkutano wa kujadili masuala mbalimbali yanayoihusu LSA, ukiwamo mradi wa ujenzi wa shule, viwanja na kituo cha michezo cha timu hiyo, utakaofanyika Kilangala, Lindi Vijijini, ambako wamepata eneo la ujenzi.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa