Home » » WANANCHI WANAOHAMIA MASHAMBANI WACHANGIA UTORO WA WANAFUNZI

WANANCHI WANAOHAMIA MASHAMBANI WACHANGIA UTORO WA WANAFUNZI

Tabia ya wananchi kuhamia mashambani na kufanya makazi ya kudumu  na kuwa  mbali na  shule  kumetajwa kuwa ni miongoni mwa  sababu zinazochangia  wilaya ya Nachingwea,mkoa wa Lindi kuwa na mahudhurio duni kwenye Shule zake.

Hayo yamesemwa na Afisa elimu wa shule za msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Nachingwea, Makwasa Bulenga kwenye taarifa yake aliyoisoma kwenye kikao cha wadau wa elimu

Amesema kuwa baadhi ya wazazi na walezi wamevihama vijiji vyao na kuhamia mashambani wakijishughulisha na Kilimo ambapo ni mbali kabisa na zilipo shule hali inayowawia vigumu watoto kuhudhuria masomo na wengine kukatiza kabisa masomo yao.

Bulenga amewataka wadau hao kufanya juhudi za makusudi za  kuishawishi jamii  kuishi katika vijiji vyenye shule  na kuwa iwapo itashindikana  na kulazikima kwenda  mashambani  wawaache watoto waendelee na masomo  badala ya kwenda nao mashambani kwani kwa kufanya hivyo ni kuonesha wazi kuwa wazazi hao hawaoni umuhimu wa elimu kwa watoto wao.

Amesisitiza kuwa  Viongozi wa Vijiji na Kata  kutumia sheria ndogo  zilizopo  kwa kuwachukulia hatua  kali wazazi na walezi ambao wanasababisha utoro kwa wanafunzi na kwamba endapo  Viongozi  watatimiza majukumu yao basi  tabia hiyo itakoma kabisa.


Akizungumzia  ukosefu wa miundombinu mbalimbali ikiwemo Madarasa,madawati matundu ya vyoo Bulenga amewataka watendaji hao kuweka  mikakati ya kuboresha  miundombinu hiyo  kwenye shule zilizo kwenye maeneo yao na kuwa idara itaendelea kuomba bajeti  ya kuongeza miundombinu  kutoka kwa Mkurugenzi wa halmashauri hiyo.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa