Home » » Mvua kubwa, upepo kutikisa

Mvua kubwa, upepo kutikisa

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza hatari ya kuwapo kwa mvua kubwa zitakazoambatana na upepo kuanzia Februari 11 hadi 13.
Taarifa iliyotolewa na TMA, inasema kiwango cha mvua hizo kinatarajiwa kuwa zaidi ya milimita 50 kwa saa 24 mfululizo.
Inaendelea kuwa mabadiliko hayo ya hali ya hewa yanasababishwa na kimbunga kilichotokea kandokando ya pwani ya Bahari ya Hindi, kilichotokea Pwani ya Somalia na Misitu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Watu wa Kongo.
Miongoni mwa mikoa iliyo katika hatari ya kukumbwa na hali hiyo, ni Dar es Salaam, Pwani, Tanga, Lindi, Mtwara, Morogoro, Mbeya, Ruvuma na Visiwa vya Unguja na Pemba.
Kutokana na hali hiyo, wakazi wa maeneo hayo na watumiaji wa bahari wametakiwa kuwa waangalifu kuepuka madhara yoyote yanayoweza kujitokeza.
Katika mvua iliyonyesha juzi, inaripotiwa kusababisha madhara Mikoa ya Dar es Salaam na Kilimanjaro.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa