Home » » CCM yadaiwa kutumia migogoro kujiimarisha

CCM yadaiwa kutumia migogoro kujiimarisha

Kwa upande wake Profesa Lipumba alisema CCM kimetumia dola ndiyo maana kimeshinda, huku akitolea mfano kata ya Kiwalala mkoani Lindi na Kiomoni mkoani Tanga

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimezidi kujizolea viti vya udiwani kata mbalimbali ikiwamo Ludewa, Tarafa ya Kimamba, wilayani Kilosa, mkoani Morogoro na Mkongoro, Wilaya ya Kigoma, mkoani Kigoma.
Juzi, CCM kilikuwa kimeshakutwaa Kata 23 huku Chadema kikinyakua vitatu wakati NCCR-Mageuzi iliambulia moja.
Kata ya Ludewa, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya Kilosa, Masalu Mayaya alimtangaza mgombea wa CCM, Subiri Mwamalila kuwa mshindi kwa kuwashinda wagombea wenzake kupitia Chadema na Cuf.
Naye Msimamizi wa Uchaguzi Kata ya Mkongoro, Wilaya ya Kigoma,, Shija Lyela alimtangaza Morani Hussein wa CCM kuwa mshindi kwa kujizolea kura 1,496 akiwashinda wapinzani wake saba waliojitokeza kuwania udiwani kata hiyo iliyokuwa ikishikiliwa na Diwani wa Chadema kuanzia mwaka 2010 ilipoanzishwa.
Kutokana na ushindi huo wa CCM katika kata 23 katika uchaguzi mdogo wa madiwani ulioshirikisha kata 27 nchini, wasomi nchini wametoa sababu nne zilizosababisha chama hicho kuibuka na ushindi kuwa ni; Utawala bora wa Sekretarieti Mpya ya CCM.
Pia, kutumia nafasi ya kujiimarisha ndani ya mgogoro wa Chadema, vyama vya upinzani kutokuwa na wanachama vijijini na kutofanyiwa maboresho kwa daftari la kudumu la wapigakura.
Wakati wasomi hao wakieleza hayo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema ushindi huo unatokana na chama hicho kuwatumikia zaidi wananchi. Kauli hiyo ya Nape ilipingwa na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba ambaye alidai kuwa chama hicho tawala kimetumia dola ndiyo maana kimefanikiwa kushinda uchaguzi huo.
Lipumba anena
Kwa upande wake Profesa Lipumba alisema CCM kimetumia dola ndiyo maana kimeshinda, huku akitolea mfano kata ya Kiwalala mkoani Lindi na Kiomoni mkoani Tanga.
“Kiomoni watu wamezuiwa kupiga kura, na Kiwalala aliyeshinda alikuwa na kesi. Pia Nec imeisaidia CCM kupata ushindi” alisema.
Profesa Lipumba alisema tabia ya chama hicho kutumia dola katika uchaguzi kinaweza kuibua vurugu nchini iwapo wananchi watachoshwa na hali hiyo, “Ili ushinde uchaguzi nchini inatakiwa uingie katika mapambano makubw ana vyombo vya dola
Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, Leticia Ghati alisema kuwa chama hicho kimeshinda kutokana na kuwa na ngome nzuri mkoani Kigoma, “Kata tuliyoshinda diwani alikuwa wa NCCR hivyo tulijua tu kuwa tutaibuka na ushindi.”
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa