Home » » Wafanyabiashara wafunga maduka kupinga unyanyasaji

Wafanyabiashara wafunga maduka kupinga unyanyasaji

Lindi.Wafanyabiashara wa Manispaa ya Lindi, wamegoma kutoa huduma kwa kufunga maduka kwa kile walichodai wamechoshwa na kero mbalimbali wanazofanyiwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Tukio hilo lilitokea juzi baada ya wafanyabiashara hao kufanya kikao na kuamua kufunga maduka kwa siku saba, ili kushinikiza TRA kuacha tabia ya kuwabugudhi.
Mwenyekiti wa umoja wa wafanyabiashara hao, Hamis Livembe alisema wameamua kufanya hivyo kutokana na kulazimishwa kutumia mashine inayouzwa Sh800,000, huku walio wengi wana mitaji midogo.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Dk Nassoro Himid alikiri kufahamu na kwamba, wanalifanyia kazi haraka ili hali hiyo isijitokeze tena ndani. Pia, juzi baadhi ya wafanyabiashara soko kuu waliamua kupanga bidhaa chini.

Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa