Home » » Kilwa Kivinje yakua kwa kasi

Kilwa Kivinje yakua kwa kasi

JIBU LA SWALI LA MBUNGE Kilwa


SERIKALI imesema suala la kupandisha hadhi mji na kuwa halmashauri ya mji mdogo linatokana na makubaliano kati ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na halmashauri husika. Hayo yalielezwa bungeni jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Kilwa Kaskazini, Suleiman Bungara (CUF).
Ghasia alisema jambo hilo linategemea kwanza wapate maombi kutoka katika halmashauri husika ambayo mpaka sasa hawajayapata, hivyo kushindwa kujua kama wana vigezo ama la.
“Mara halmashauri husika itakapoleta maombi kwetu sisi tutajua kama eneo husika lina vigezo vya kupandishwa hadhi na kuwa mji mdogo na kukamilisha zoezi hilo kwa haraka,” alisema Ghasia.
Alikiri ipo kasi ya ukuaji wa idadi ya watu katika mji wa Kilwa Kivinje ambayo inaleta changamoto katika utoaji wa huduma za jamii katika eneo hilo.
Alisema kwa kuzingatia hilo, serikali ilitangaza mji huu kuwa eneo la mipango kupitia Tangazo la Serikali Na. 176, la Agosti 9, mwaka 1996 ili kuzuia ukuaji holela, kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha huduma za jamii.
Katika swali lake mbunge huyo alitaka kujua ni lini zoezi la kukamilisha Kilwa Kivinje litakamilika, lililoulizwa kwa niaba yake na Mbunge wa Ole, Rajabu Kasim Mbarouk.

CHANZO;TANZANIA DAIMA

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa