Home »
 » Kilwa Kivinje yakua kwa kasi 
 
Kilwa Kivinje yakua kwa kasi 
| 
| 
JIBU LA SWALI LA MBUNGE Kilwa 
 |  | 
 | 
 | 
  
    | 
SERIKALI imesema suala  la kupandisha hadhi mji na kuwa 
halmashauri ya mji mdogo linatokana na  makubaliano kati ya Tawala za 
Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) na  halmashauri husika.
  Hayo yalielezwa bungeni  jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu 
Tawala za Mikoa na Serikali za  Mitaa (TAMISEMI), Hawa Ghasia, alipokuwa
 akijibu swali la msingi la Mbunge wa  Kilwa Kaskazini, Suleiman Bungara
 (CUF).Ghasia alisema jambo  hilo linategemea kwanza wapate maombi kutoka 
katika halmashauri husika ambayo  mpaka sasa hawajayapata, hivyo 
kushindwa kujua kama wana vigezo ama la.
 “Mara halmashauri  husika itakapoleta maombi kwetu sisi tutajua kama 
eneo husika lina vigezo vya  kupandishwa hadhi na kuwa mji mdogo na 
kukamilisha zoezi hilo kwa haraka,”  alisema Ghasia.
 Alikiri ipo kasi ya  ukuaji wa idadi ya watu katika mji wa Kilwa 
Kivinje ambayo inaleta changamoto  katika utoaji wa huduma za jamii 
katika eneo hilo.
 Alisema kwa kuzingatia  hilo, serikali ilitangaza mji huu kuwa eneo la
 mipango kupitia Tangazo la  Serikali Na. 176, la Agosti 9, mwaka 1996 
ili kuzuia ukuaji holela, kuchochea  ukuaji wa uchumi na kuboresha 
huduma za jamii.
 Katika swali lake  mbunge huyo alitaka kujua ni lini zoezi la 
kukamilisha Kilwa Kivinje  litakamilika, lililoulizwa kwa niaba yake na 
Mbunge wa Ole, Rajabu Kasim  Mbarouk.
 
 CHANZO;TANZANIA DAIMA
 
 |  | 
 
 
0 comments:
Post a Comment