Home » » Viongozi Halmashauri Ruangwa lawamani

Viongozi Halmashauri Ruangwa lawamani

Ruangwa.Wanachama wa Chama cha Ushirika cha Msingi Luchelegwa, Wilaya ya Ruangwa, Mkoa wa Lindi, wamelalamikia uongozi wa halmashauri hiyo kwa kuwaondoa madarakani watendaji wao kwa madai ya kutumia gari la Chuo Kikuu cha Ushirika cha Mkoa Ilulu, kusambaza fedha za kununulia korosho.
Akizungumza kwa niaba ya wakulima na wanachama wa chama hicho, Somoe Liuna alisema wakulima wa korosho hawatambui uongozi uliowekwa na viongozi wa halmashauri ya wilaya hiyo. (Mwanja Ibadi)
kwa maslai yao ya kisiasa.
Somoe alisema kitendo hicho cha halmashauri kuingia uhuru wa vyama vya ushirika ni kuvunja sheria ya ushirika kifungu 20 cha mwaka 2000 na kinawakatisha tamaa wakulima kujiunga kwenye vyama hivyo.
Fabiani Nguli diwani wa kata ya Chinongwe alisema kuwa mgogoro wa chama cha ushirika Luchelengwa umetengenezwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Ruangwa Issa Libaba kwa lengo la kukidhahofisha chama hicho chenye mafanikio makubwa ya kiuchumi.
Nguli alisema mwenyekiti huyo anatumia nafsi yake vibaya kwa maslai yake binafsi anasahau maslai ya umma maana mgogoro alioutengeneza unalengo la kuwaumiza wakulima wasiona hatia wasiuze mazao yao kwa wakati.
Alisema chama cha ushirika Luchelegwa kimepata mafanikio makubwa chini ya uongozi uliondolewa na mwenyekiti huyo hali ambayo wakulima na wanachama hawaweza kukubalina na maamuzi yake.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya Ruangwa Issa Libaba alikiri kuwepo kwa mgogoro katika chama hicho lakini alikanusha kuwa mgogoro huo haujasababishwa na viongozi na watendaji wa halmashauri hiyo.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa