Home » » Kutoelewana baina ya watendaji wa vijiji na wanasiasa kikwazo cha maendeleo Nachingwea

Kutoelewana baina ya watendaji wa vijiji na wanasiasa kikwazo cha maendeleo Nachingwea


Migogoro, mivutano na malumbano ya mara kwa mara ya watendaji  wakuu wa kata na vijiji na viongozi wa siasa imetajwa kuwa  ni kati ya sababu zinazofanya baadhi ya miradi  ya maendeleo kwenye halmashauri ya wilaya ya  Nachingwea kutotekelezwa  kwa wakati.
 Akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa kipindi cha mwezi aprili na juni mwaka huu  kwenye kikao cha Baraza la madiwani la halmashauri hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashairi ya wilaya ya Nchingwea, Afisa mipango,James Mbakile amesema kuwa hali hiyo inafanya watendaji hao kukosa  muda wa  kusimamia miradi hiyo  na kwa kiasi kikubwa  kuwakatisha tamaa na kuwafanya wakose ari na kujituma katika uwajibikaji.
Mbakile ametaja changamoto nyingine kuwa ni pamoja na baadhi ya wakandarasi kutokuwa wakweli na waaminifu katika utekelezaji wa miradi ya ujenzi  hivyo kuchelewesha kazi na baadhi ya kazi kuwa chini ya viwango.
Na katika kukabiliana na changamoto hiyo halmashauri imeendelea kutangaza kazi kwenye vyombo mbalimbali vya habari ili kuwapata wakandarasi wa nje ya wilaya ili kuleta ushindani katika kutekeleza  miradi mingi ya maendeleo iliyopo kwenye halmashauri hiyo.
Pia amesema sababu nyingine ni kuchelewa sana kwa ruzuku ya maendeleo toka Serikali kuu ambako huathiri kwa kiwango kikubwa kuanza kwa utekelezaji wa shughuli za maendeleo.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa