Home » » RC AIPA SOMO NHIF

RC AIPA SOMO NHIF



na Mwandishi wetu, Lindi
MKUU wa Mkoa wa Lindi, Ludovick Mwananzila, ameutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kujikita zaidi kwenye uhamasishaji zaidi hususan maeneo ya vijijini ambako mahitaji ya huduma za afya kwa wananchi walio wengi yako huko.
Mwananzila alitoa ushauri huo kwenye maadhimisho ya Siku ya Afya ya Akili ambayo kitaifa yamefanyika mkoani hapa.
“…hakikisheni kasi ya uhamasishaji inaongezeka na wanachi wengi wanajiunga kwenye mfuko huu. Haiwezekani kwa Mkoa wa Lindi uwe na wanachama asilimia 5.4 ya kaya 194,424 ,hii ni ishara tosha kuwa wananchi hawajapata elimu ya dhana na umuhimu wa mfuko huu,” alisema mkuu huyo wa mkoa ambaye alimwakilisha Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kwenye maadhimisho hayo.
Ameutaka mfuko huo kujipanga vema kukabiliana na changamoto za huduma za matibabu zilizopo kwenye mkoa huo hususan uhaba wa dawa katika vituo vya matibabu.
Mwakilishi wa NHIF Ofisi ya Mkoa wa Lindi, Fortunata Kulaya, alisema changamoto kubwa iko kwenye matumizi ya fedha za tele kwa tele na zinazolipwa na MHIF kutokutumiwa kwa malengo yaliyokusudiwa, hivyo kudhoofisha mwitikio wa wananchi kujiunga na Mifuko ya Afya ya Jamii (CHF).
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa