Home » » WATOTO RUANGWA WAKUMBWA NA UDUMAVU

WATOTO RUANGWA WAKUMBWA NA UDUMAVU

na Happy Mollel, Ruangwa
UZALISHAJI duni wa vyakula wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, unaoambatana na ukosefu wa utaalamu wa kutumia vyakula vichache vilivyopo, umesababisha watoto wengi kukumbwa na tatizo la utapiamlo na udumavu.
Changamoto hiyo ilitolewa na Ofisa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto wa Wilaya, Suleman Mohamed, na kuongeza kuwa Ruangwa ni moja kati ya wilaya zinazosumbuliwa na tatizo la lishe.
“Bila kuficha wilaya yetu bado ina changamoto kubwa ukilinganisha na wilaya nyingine…tatizo la lishe ni kubwa na hii ni kutokana na familia nyingi za huku kukosa uhakika wa kupata chakula kwa milo yote mitatu kama tulivyozoea,” alisema.
Alibainisha kuwa sababu nyingine inayochangia kuwapo kwa utapiamlo ni kukosekana kwa elimu sahihi ya namna ya kutumia vyakula vya asili vikiwemo vile vyenye virutubisho vingi.
Akitoa ufafanuzi juu ya tatizo la lishe wilayani hapa, Ofisa Lishe wa Wilaya, Vaileth Richard, alisema mbali na kukosekana kwa utaalamu wa kuvitumia vyakula vichache vilivyopo, ofisi yake tayari imeshajiwekea mikakati ya kuongeza maeneo ya kilimo kwa mazao ya chakula, ili kukabiliana na ukosefu wa vyakula.
Chanzo: Tanania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa