Eneo la tukio
Ingawa vifaa vilikuwa duni  kazi ya uokoaji iliendelea
Watu walifanya kazi kufa na kupona
Baadhi ya maiti akitolewa eneo la tukio
Mbunge wa Ruangwa  Mh. Kassim Majaliwa akiwa  eneo la tukio  sambamba na Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Agness Hokororo
RPC  wa Lindi  MWAKAJINGA na OCD wa RUNGWA V.P MAJANI wakitoa pole  kwa wafiwa na shukrani kwa waokoaji
Maafa makubwa yametokea jana katika kijiji cha Mnacho maeneo ya Nandagala wilayani Ruangwa (pichani) baada ya wachimba madini saba kufukiwa na kifusi cha  mwamba. Kazi ya uokozi ilianza jana  majira saa 9 jioni na imechukua masaa zaidi ya 12  kutokana na uduni wa vifaa vya uokoaji. Katika tukio hilo watu saba wamepotea maisha na miili yote imepatikana . Majina ya Marehemu wa kadhia hiyo ni Chakoda - 20 mkazi wa Dar es salaam, Nyang'ana - 42 mkazi wa Musoma, Uwesu Bakari - 25 mkazi wa Rondo Lindi, Mohamedi Omary - 28 mkazi wa Morogoro, Bakari Rashidi Liganga - 26 mkazi Chunyu Ruangwa, Adam Sayai  Mkazi wa bunda  na Rashid Hamis Yasin wa Nachingwea
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment