 Maiti  za wachimbaji wadogo wa Madini katika Machimbo ya Madini katika Kata ya  Nandagala Wilayani  Ruangwa Mkoani Lindizikiwa zimetolewa tayari kwa  utambuzi. Watu saba walifukiwa na Kifusi na kupoteza maisha katika moja  ya Mashimo ya Mgodi huo juzi.
Maiti  za wachimbaji wadogo wa Madini katika Machimbo ya Madini katika Kata ya  Nandagala Wilayani  Ruangwa Mkoani Lindizikiwa zimetolewa tayari kwa  utambuzi. Watu saba walifukiwa na Kifusi na kupoteza maisha katika moja  ya Mashimo ya Mgodi huo juzi.  Zoezi  la uokoaji lililokuwa likifanywa na wananchi wa Kata ya Ndagala yalipo  Machimbo ya Madini katika Kata hiyo Wilayani  Ruangwa Mkoani Lindi  ukiendelea.
Zoezi  la uokoaji lililokuwa likifanywa na wananchi wa Kata ya Ndagala yalipo  Machimbo ya Madini katika Kata hiyo Wilayani  Ruangwa Mkoani Lindi  ukiendelea. 
Kikosi cha wananchi cha Uokoaji kikiwa kimewafikia watu hao waliofukiwa na kifusi. 
Na Abdulaziz video
Zoezi  la kufukua  Maiti za watu waliofunikwa  na kifusi katika Machimbo ya  Madini katika Kata ya Nandagala Wilayani  Ruangwa Mkoani Lindi jana  limekamilika leo asubuhi  huku  wakifanikiwa kuzipata maiti zote 7
Akiongea na mtandao huu,Diwani wa Kata hiyo,Andrew Chikongwe alibainisha kuwa kazi ya kufukua kifusi hicho imechukua muda mrefu kufuatia na kuwepo kwa zana duni za kufukua Mchanga hali iliyofanya kazi hiyo kuwa Ngumu kuanzia jana saa 9 jioni hadi leo asubuhi
Chikongwe aliwataja Marehemu hao ni Nyang'ana Mkelecha,Mkazi wa Musoma,Mohamed Omari Fondogoro,Mkazi wa Morogoro,Bakari Liganga mkazi wa Chunyu Ruangwa,Rajab maarufu ROGER Mkazi wa Musoma,Uwesu Bakari Abeid mkazi wa Rondo,Chakoda Mkazi wa Dar na Rashid Ally maarufu BADE Mkazi wa Masasi mkoani Mtwara
Akiongea na mtandao huu,Diwani wa Kata hiyo,Andrew Chikongwe alibainisha kuwa kazi ya kufukua kifusi hicho imechukua muda mrefu kufuatia na kuwepo kwa zana duni za kufukua Mchanga hali iliyofanya kazi hiyo kuwa Ngumu kuanzia jana saa 9 jioni hadi leo asubuhi
Chikongwe aliwataja Marehemu hao ni Nyang'ana Mkelecha,Mkazi wa Musoma,Mohamed Omari Fondogoro,Mkazi wa Morogoro,Bakari Liganga mkazi wa Chunyu Ruangwa,Rajab maarufu ROGER Mkazi wa Musoma,Uwesu Bakari Abeid mkazi wa Rondo,Chakoda Mkazi wa Dar na Rashid Ally maarufu BADE Mkazi wa Masasi mkoani Mtwara
Chanzo: Mrokim blog 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment