Na. Mwandishi Wetu
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri
 Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu, Mhe. Dkt. Abdallah
 Possi ameitaka jamii kuzingatia haki na usawa kwa watu wenye ulemavu nakuondokana na imani potofu za kuona watu wenye ulemavu hawana uwezo wa kufanya shughuli za maendeleo.
Mhe. Possi ameyasema
 hayo kwa nyakati tofauti alipotembelea Vituo na Shule zinazohudumia 
watu wenye mahitaji maalum vya Nandanga, Rasi Bula, Shule ya msingi 
Nyangao mkoani Lindi pamoja na makazi ya wenye ulemavu na Ukoma ya 
Mkaseka, Chuo cha wenye Ulemavu cha Mtapika, shule ya Lulindi na Masasi 
mkoani Mtwara.
Katika ziara hiyo Mhe.Possi 
alisisitiza jamii zibadili mitazamo hasi juu ya masuala ya haki na usawa
 kwa watu wenye ulemavu kwa kuwashirikisha katika shughuli zote na 
kuwapa vipaumbele vya fursa sawa.
“Ninasisitiza jamii ibadili 
mitazamo dhaifu juu ya haki na usawa wa kuwashirikisha watu wenye 
ulemavu kwani wana uwezo wa uzalishaji endapo tutawapa fursa sawa kama 
ilivyokuwa kwa wakina mama walipoachwa nyuma muda mrefu ila jamii imeona
 fursa ndani yao, iwe hivyo hivyo kwa watu wenye ulemavu” alisema.
Aidha Waziri Possi ameweka mkazo juu ya kuwahusisha na kutokuwaona kuwa ni kundi la kuachwa nyuma na kama tegemezi.
“sheria zipo wazi kabisa 
zinazotuelekeza juu ya haki na usawa kwa watu wenye ulemavu kwa mujibu 
wa matakwa ya Sheria ya watu wenye Ulemavu namba 9 ya mwaka 2010 
inayoeleza haki za watu wenye Ulemavu kuwahudumia kwa haki na usawa na 
kuboresha maeneo muhimu ikiwemo fursa za kielimu, ajira, kiuchumi na 
kijamii,” alieleza.
Kwa upande wake, Mkuu
 wa Wilaya ya Ruangwa Mhe. Joseph Mkirikiti alikiri kuyapokea yote 
aliyoeleza Mhe.Waziri katika ziara yake na kuipongeza Serikali kwa 
juhudi za kuisaidia jamii bila kujali hali zao na tofauti zao.
“Ninaipongeza Serikali ya 
Awamu ya Tano inayowajali wanyonge na kujali haki zao pamoja na mhe. 
Waziri kwa kuona umuhimu wa kututembelea wana Ruangwa na tunaahidi 
kukuweka katika kumbukumbu zetu maana umewagusa wakazi wa Mtwara 
hususani wazee na watu wenye ulemavu.”Alisisitiza Mkuu wa Wilaya hiyo.
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment