Home » » Zambi aagiza oparesheni UKUTA isifike Lindi

Zambi aagiza oparesheni UKUTA isifike Lindi


Na Godfriend Mbuya

Mkuu wa Mkoa wa Lindi Godfrey Zambi amesema maandamano na mikutano ya hadhara itakayojumuisha viongozi wa kitaifa iliyotangazwa na CHADEMA haitaruhusiwa kufanyika katika mkao wake tarehe 01.09.2016.

Zambi ameyasema hayo ofisini kwake ikiwa ni siku chache tangu CHADEMA kutangaza maazimio ya chama chao kwamba wataanza oparesheni ya kuelimisha wananchi kuhusu masuala ya kidemokrasia kwa kufanya oparesheni nchi nzima iliyopewa jina la UKUTA ikiwa na maana Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania.

''Rais Dkt. John Magufuli ameshatoa agizo la kusitisha maandamano , hivyo hakuna mtu au kikundi chochote cha siasa ambacho kinaruhusiwa kufanya maandamano siku hiyo ya tarehe 01.09.2016 na ninamwagiza RPC Mkoa wa Lindi kuhakikisha hakuna maadamano siku hiyo na watu waendelee na kazi zao kama kawaida'' Amesema Zambi.

Aidha Zambi amesema mikutano ambayo imezuiwa ni ile ya viongozi kutoka mikoa mingine na kwenda Lindi , lakini kama ni wabunge wa Lindi na madiwani wakitaka kufanya mikutano ya hadhara wafanye katika maeneo yao.

''Wabunge wa Lindi na madiwani wanaruhusiwa kufanya mikutano lakini siyo mtu atoke Arusha au Mbeya kuja kufanya maandamano na mikutano ya hadhara Lindi'' Amesisitiza Zambi.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa