Home » » KITUO CHA MABASI MASASI SASA SAFI, WAHUSIKA WAAMKA BAADA YA KUMULIKWA

KITUO CHA MABASI MASASI SASA SAFI, WAHUSIKA WAAMKA BAADA YA KUMULIKWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Stendi Kuu ya Mabasi yaendayo Mikoani Wilayani Masasi yaendelea Kuboreshwa kwa kufanyiwa Usafi wa Hali yajuu.

Leo hii Baada ya Kamera ya Lindiyetu.com kupita majira ya asubuhi ilikuta eneo hilo ambalo hapo jana lilikuwa limetapakaa Uchafu wa Kila aina likiwa Safi Kabisa.

KAMA ULIPITWA NA POST HIYO BOFYA HAPA KUANGALIA UCHAFU ULIOKUWEPO 



Hii inaonesha kabisa Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Masasi amedhamiria kuepuka aibu ambayo ilikuwa inakuja siku za usoni kwani eneo hilo lipo katikati ya Mji huo hivyo kuonekana kirahisi na Kuleta Picha mbaya.



Tunaipongeza Halmashauri ya Mji ambayo imelichukua jambo hili kwa Umakini mkubwa hadi kufikia Kuweka Greda ambalo lilikutwa likifanya kazi ya kuendelea kuweka Mazingira sawia katika Stend kuu hiyo.



UNAWEZA BOFYA PLAY KUTAZAMA VIDEO HAPO CHINI
HONGERENI SANA...!!!

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa