Wananchi
 wote mnakaribishwa kutembela banda la Wizara ya Fedha na taasisi zilizo
 chini yake ikiwemo UTT AMIS, Mfuko wa Pensheni PPF, GPSA na UTT PID 
uwanja wa maonesho ya kilimo ya Nane Nane Kitaifa Ngongo mkoani Lindi.
Mtendaji
 Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat 
Mwambega akipokea fomu ya kujiunga na Mfumo wa Amana inayotolewa na 
Mfuko wa Pensheni wa PPF kutoka kwa Afisa Masoko wa Mfuko huo Nelusigwe 
Mwalugaja wakati alipotembelea banda la Wizara ya Fedha. Wa kwanza kulia
 ni Mhasibu kutoka PPF.
Mtendaji
 Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat 
Mwambega akiongea na Afisa Msoko na Uhusiano, Rahimu Mwanga kutoka 
taasisi ya UTT AMIS kwenye Uwanja wa  maonesho ya Kilimo ya Nane Nane 
Ngongo Mkoani Lindi.
Afisa
 Masoko na Uhusiano, Rahimu Mwanga kutoka taasisi ya UTT AMIS akiongea 
na baadhi ya wageni wakijionea kazi mbalimbali zinazofanywa na taasisi 
hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane uwanja wa Ngongo Mkoani 
Lindi.
Mhasibu
 kutoka Idara ya Pensheni Wizara ya Fedha, Imelda Mzatulla akiongea na 
baadhi ya wageni waliofika kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na 
Wizara ya Fedha wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane uwanja wa 
Ngongo Mkoani Lindi.
Afisa
 Masoko Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nelusigwe Mwalugaja (kulia) akiongea 
na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na 
Ushirika Anne Assenga (kushoto) wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane 
Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
Afisa
 Masoko na Uhusiano wa Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundo Mbinu 
(UTT PID), Kilave Atenaka akifafanua jambo kwa baadhi ya wageni 
waliotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane
 Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi. 
Mtaalamu
 wa  Mawasiliano kutoka Program ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za 
Umma (PFMRP) Wizara ya Fedha, Alexander Iweikiza akimsikiliza Mtendaji 
Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat Mwambega
 alipotembelea Banda la Wizara hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane
 Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
Mhasibu
 kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF, Anne Paul akiwapa zawadi wanafunzi wa 
shule ya msingi Tulieni iliyopo kata ya Mnazi Mmoja walipotembelea banda
 la maonesho mfuko huo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kitaifa
 yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
Pichani
 juu na chini ni baadhi ya wageni waliofika banda la Wizara ya Fedha 
kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Fedha na taasisi 
zake.(Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Lindi).
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment