01.
Wananchi wote mnakaribishwa kutembela banda la Wizara ya Fedha na taasisi zilizo chini yake ikiwemo UTT AMIS, Mfuko wa Pensheni PPF, GPSA na UTT PID uwanja wa maonesho ya kilimo ya Nane Nane Kitaifa Ngongo mkoani Lindi.
04
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat Mwambega akipokea fomu ya kujiunga na Mfumo wa Amana inayotolewa na Mfuko wa Pensheni wa PPF kutoka kwa Afisa Masoko wa Mfuko huo Nelusigwe Mwalugaja wakati alipotembelea banda la Wizara ya Fedha. Wa kwanza kulia ni Mhasibu kutoka PPF.
05
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat Mwambega akiongea na Afisa Msoko na Uhusiano, Rahimu Mwanga kutoka taasisi ya UTT AMIS kwenye Uwanja wa  maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Ngongo Mkoani Lindi.
06
Afisa Masoko na Uhusiano, Rahimu Mwanga kutoka taasisi ya UTT AMIS akiongea na baadhi ya wageni wakijionea kazi mbalimbali zinazofanywa na taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
07
Mhasibu kutoka Idara ya Pensheni Wizara ya Fedha, Imelda Mzatulla akiongea na baadhi ya wageni waliofika kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Fedha wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
08
Afisa Masoko Mfuko wa Pensheni wa PPF, Nelusigwe Mwalugaja (kulia) akiongea na Mkurugenzi wa Mafunzo ya Kilimo kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Anne Assenga (kushoto) wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
09
Afisa Masoko na Uhusiano wa Taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundo Mbinu (UTT PID), Kilave Atenaka akifafanua jambo kwa baadhi ya wageni waliotembelea banda la taasisi hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
10
Mtaalamu wa  Mawasiliano kutoka Program ya Maboresho ya Usimamizi wa Fedha za Umma (PFMRP) Wizara ya Fedha, Alexander Iweikiza akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma ya Ununuzi Serikalini (GPSA), Josephat Mwambega alipotembelea Banda la Wizara hiyo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
11
Mhasibu kutoka Mfuko wa Pensheni wa PPF, Anne Paul akiwapa zawadi wanafunzi wa shule ya msingi Tulieni iliyopo kata ya Mnazi Mmoja walipotembelea banda la maonesho mfuko huo wakati wa maonesho ya Kilimo ya Nane Nane Kitaifa yanayoendelea uwanja wa Ngongo Mkoani Lindi.
12
Pichani juu na chini ni baadhi ya wageni waliofika banda la Wizara ya Fedha kujionea kazi mbalimbali zinazofanywa na Wizara ya Fedha na taasisi zake.(Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Lindi).
13
14