Home » » MAMA SALMA KIKWETE AZURU LINDI/ AHUTUBIA MKUTANO MKUBWA LINDI MANISPAA, AKABIDHI BATI 100 NA VYOMBO VYA BENDI SHULE YA SEKONDARI ANGAZA

MAMA SALMA KIKWETE AZURU LINDI/ AHUTUBIA MKUTANO MKUBWA LINDI MANISPAA, AKABIDHI BATI 100 NA VYOMBO VYA BENDI SHULE YA SEKONDARI ANGAZA


Mke wa Rais na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Lindi Mjini Mama Salma Kikwete akipokewa na Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mheshimiwa Mwantumu Mahiza mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Lindi tarehe 15.3.2015 kuanza ziara ya kikazi ya siku 5 kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipokea kadi kutoka kwa aliyekuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Kata ya Tulieni Mjini Lindi wa Chama Cha Wananchi (CUF) Ndugu Shaibu Rajabu Matola (Kikaptura) aliyeamua kukihama chama hicho na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wakati wa mkutano mkubwa uliofanyika kwenye Kata ya Mikumbi tarehe 16.3.2015.
Mke wa Rais na Mjumbe wa NEC Taifa Mama Salma Kikwete akikabidhi bati 100 na vifaa vya bendi kwa uongozi wa Shule ya Sekondari Angaza iliyoko katika Manispaa ya Lindi tarehe 16.3.2015. Anayepokea kwa niaba ya shule hiyo ni Mkuu wa Shule Mwalimu Upendo Muro (wa tano kutoka kulia) akiwa pamoja na Ndugu Ashimun Mzava, Afisa Elimu Sekondar, Manispaa Lindi wa nne kutoka kulia) na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo. Aliyesimama wa kwanza kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Lindi Bwana Abdallah Ulega.

    Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa