Home » » MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHI SAMPULI ZA MADAWATI KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA MADARASA YA AWALI KATIKA MANISPAA YA LINDI MJINI

MAMA SALMA KIKWETE AKABIDHI SAMPULI ZA MADAWATI KATIKA SHULE ZA MSINGI KWA MADARASA YA AWALI KATIKA MANISPAA YA LINDI MJINI


Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo,WAMA, Mama Salma Kikwete akisalimiana na Afisaelimu wa Mkoa wa Lindi Ndugu Gift Kyando mara baada ya kuwasili kwenye viwanja wa Shule ya Msingi Rahaleo iliyoko Manispaa ya Lindi Mjini kwa ajili ya kukabidhi sampuli za madawati aliyoyatoa kupitia taasisi yake kwenye Shule za Msingi kwa ajili ya madarasa ya awali katika Manispaa ya Lindi Mjini tarehe 15.12.2014.
Baadhi ya wanafunzi wanaosoma Madarasa ya Awali katika Shule ya Msingi ya Rahaleo wakiwa pamoja na walimu wao wakipiga makofi ikiwa ni ishara ya kumpokea Mke wa Rais Mama Salma Kikwete wakati anawasili shuleni hapo tarehe 15.12.2014.
Sampuli za madawati yaliyotolewa na Mwenyekiti wa WAMA na Mke wa Rais Mama Salma Kikwete kwenye Shule za Msingi kwa ajili ya madarasa ya awali katika Manispaa ya Lindi Mjini tarehe 15.12.2014.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya WAMA, Mama Salma Kikwete akitoa hotuba fupi kabla ya kukabidhi sampuli za madawati yaliyotolewa na Taasisi yake kwenye shule za Msingi kwa ajili ya madarasa ya awali katika Manispaa ya Lindi Mjini kwenye sherehe fupi iliyofanyika kwenye Shule ya Msingi Rahaleo tarehe 15.12.2014.
Mke wa Rais na Mwenyekiti wa WAMA, Mama Salma Kikwete akikabidhi sampuli za madawati yaliyotolewa na Taasisi ya WAMA kwa Afisaelimu wa Mkoa wa Lindi Ndugu Gift Kyando kwa ajili ya Shule za Msingi zenye madarasa ya awali katika Manispaa ya Lindi Mjini. Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye Shule ya Msingi ya Rahaleo tarehe 15.12.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akizungumza na binti Naida Seleman anayesoma darasa la awali katika Shule ya Msingi ya Rahaleo mara baada ya Mama Salma kukabidhi sampuli za madawati aliyoyatoa kwenye Shule za Manispaa ya Lindi Mjini tarehe 15.12.2014.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akipiga picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa Mkoa wa Lindi, wanafunzi wa madarasa ya awali wanaosoma katika Shule ya Msingi Rahaleo na walimu wao wakati wa sherehe ya kukabidhi sampuli za madawati tarehe 15.12.2014. PICHA NA JOHN LUKUWI.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa