Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
WAZIRI wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Mhandisi Christopher Chiza,
amesema njia pekee na nzuri ya kumsaidia mkulima ni kuhakikisha mfumo
wa stakabadhi ghalani unaboresha.
Chiza aliyasema hayo juzi kwenye katika siku ya Korosho Tanzania, iliyofanyika viwaja vya Ngongo mkoani Lindi.
Alisema kuwa njia nzuri ya kuweza kumsaidia mkulima ni kuhakikisha kwamba taratubu zote zinaboreshwa.
“Muda mfupi uliopita tu nimejifunza msamiati mpya, nilizoea neno
kangomba leo nimesikia chomachoma kwenye ufuta, asubuhi niliuliza mwaka
huu sijasikia kelele nyingi za soko la korosho sababu yake kubwa ni
nini?
“Nilipata majibu kuwa sababu yake kubwa ni kwamba tulipotangaza bei
dira ya korosho, fedha zilipatikana kwa wakati, kwa hiyo mkulima akipata
fedha zake hakutakuwepo na migogoro,” alisema.
Waziri Chiza aliongeza kuwa wakulima si kwamba hawaupendi mfumo wa
stakabadhi ghalani, isipokuwa hawapendi mambo yanayojitokeza ya
ucheleweshaji wa fedha.
“Mimi naamini kuwa mfumo mzima ni mzuri, tunachotakiwa sasa kutafuta
yale yote yanayowauzi wakulima katika mfumo huu ili yaboreshwe,”alisema.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment