Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KATIBU
wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi,
Nape Nnauye, amewataka wanasiasa wanaofanya mikutano ya hadhara katika
majimbo yao kuacha mara moja kwani ni kuvunja sheria iliyowekwa na
serikali.
Nape aliyasema hayo katika Kijiji cha Rondo mkoani Lindi juzi, baada
ya kuulizwa na waandishi wa habari, kwanini baadhi ya wabunge wa CCM,
akiwemo mbunge wa Newala ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Utawala Bora, George Mkuchika, wanafanya mikutano ya hadhara katika
majimbo yao wakati serikali ilipiga marufuku mikusanyiko na mikutano ya
hadhara kwa mikoa ya Lindi na Mtwara.
Nape alisema kuwa sheria ya kutofanya mikutano ilipitishwa na serikali na ni halali na kama mtu anaivunja si sawa, anakiuka.
“Hii sheria ya kutofanya mikutano ilipitishwa na serikali na ni
halali, sasa kama kuna mtu anaivunja si sawa sawa, kama mnakumbuka hata
mimi nilivyokuja Mtwara watu wa chama waliniandalia kufungua mashina…Wao
walidhani kufungua mashina na kuondoka, lakini kwa sababu ya ‘impact’
ya Katibu Mwenezi anakuja kikazi, wakaona ingejaza watu na ingevunja
sheria, waliponiambia tu niliwaambia msifanye mikutano na tulikwenda
kufanya kikao cha ndani na zile bendera sikwenda kuzipandisha kwenye
mashina, lakini nikawagawia watu wakaenda kupandisha.
“Uzuri na ubaya wa hii sheria sitaki sana kuingilia ndani kuijadili,
lakini wakati nilipokuja Mtwara kama mnakumbuka, nilisema kuendelea na
sheria hii ni kubaka demokrasia, kwa sababu hatuwezi kuzuia watu
wasifanye shughuli zao za kisiasa kwa muda mrefu kiasi hicho, walizuia
kwa sababu fulani, kulikuwa na vurugu Mtwara wakati ule juu ya mambo ya
gesi sasa zimeisha,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment