Home » » CCM WATAKIWA KUFUATA SHERIA

CCM WATAKIWA KUFUATA SHERIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape NnauyeKATIBU wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amewataka wanasiasa wanaofanya mikutano ya hadhara katika majimbo yao kuacha mara moja kwani ni kuvunja sheria iliyowekwa na serikali.
Nape aliyasema hayo katika Kijiji cha Rondo mkoani Lindi juzi, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari, kwanini baadhi ya wabunge wa CCM, akiwemo mbunge wa Newala ambaye pia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, George Mkuchika, wanafanya mikutano ya hadhara katika majimbo yao wakati serikali ilipiga marufuku mikusanyiko na mikutano ya hadhara kwa mikoa ya Lindi na Mtwara.
Nape alisema kuwa sheria ya kutofanya mikutano ilipitishwa na serikali na ni halali na kama mtu anaivunja si sawa, anakiuka.
“Hii sheria ya kutofanya mikutano ilipitishwa na serikali na ni halali, sasa kama kuna mtu anaivunja si sawa sawa, kama mnakumbuka hata mimi nilivyokuja Mtwara watu wa chama waliniandalia kufungua mashina…Wao walidhani kufungua mashina na kuondoka, lakini kwa sababu ya ‘impact’ ya Katibu Mwenezi anakuja kikazi, wakaona ingejaza watu na ingevunja sheria, waliponiambia tu niliwaambia msifanye mikutano na tulikwenda kufanya kikao cha ndani na zile bendera sikwenda kuzipandisha kwenye mashina, lakini nikawagawia watu wakaenda kupandisha.
“Uzuri na ubaya wa hii sheria sitaki sana kuingilia ndani kuijadili, lakini wakati nilipokuja Mtwara kama mnakumbuka, nilisema kuendelea na sheria hii ni kubaka demokrasia, kwa sababu hatuwezi kuzuia watu wasifanye shughuli zao za kisiasa kwa muda mrefu kiasi hicho, walizuia kwa sababu fulani, kulikuwa na vurugu Mtwara wakati ule juu ya mambo ya gesi sasa zimeisha,” alisema.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa