Home » » BODI ZA MAZAO ZATAKIWA KUTATUA KERO ZA WAKULIMA

BODI ZA MAZAO ZATAKIWA KUTATUA KERO ZA WAKULIMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Bodi za mazao nchini zimetakiwa kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wakulima ili kuwajengea uwezo wa kuzalisha kwa wingi na kufikia mahitaji ya soko la ndani na nje.
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Injinia Christopher Chiza aliyasema hayo wakati akifungua mkutano mkuu wa wadau wa korosho Tanzania uliyofanyika wilayani Masasi, mkoani Mtwara.
Alisema bodi hizo zinatakiwa kutatua matatizo ya wakulima yanayowakwaza na kushindwa kufikia malengo ya uzalishaji.
Chiza alisema hivi sasa kuna mwanya mkubwa kati ya bodi, halmashauri za wilaya na miji, mifuko ya pembejeo na wakulima hali ambayo kimsingi inamuumiza zaidi mkulima.
Waziri huyo alisema sababu ya mwanya huo ni wakulima kutoshirikishwa katika uamuzi, kama kukokotoa hesabu za uendeshaji zinazohusu ununuzi, gharama za matumizi na malipo ya majaliwa ambayo ni kiini cha mafanikio kwa mkulima.
Alisema wakulima wako tayari kuzalisha bidhaa za mazao, lakini tatizo ni viongozi wa bodi zao kushindwa kutekeleza matakwa ya wakulima na kutanguliza masilahi yao binafsi.
“Ili mkulima apewe matumaini ya kuzalisha mazao kwa tija, lazima bodi ziwe mstari wa mbele katika utendaji wa majukumu yake kwa ufanisi na uaminifu zaidi na kutii sheria ya ushirika na kanuni za kutamsaidia mkulima,” alisema.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania, Anna Abdallah, ameiomba Serikali kuwaajiri watafiti vijana ili kuchukua nafasi zilizoachwa wazi na watafiti wastaafu.
Alisema mfano kituo cha utafiti cha Naliendele kilichopo mkoani Mtwara, ambapo kwa sasa kituo hicho kimebaki na mtafiti mmoja anayefanya kazi kwa mkataba baada ya muda wake wa utumishi kukoma
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa