Home » » TASO YAKANUSHA MADAI YA NANENANE

TASO YAKANUSHA MADAI YA NANENANE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Uongozi wa Chama cha Wakulima (Taso) umekanusha madai yanayotolewa na baadhi ya watu kuwa sherehe za wakulima na maonyesho ya kilimo za Nanenane, hazitafanyika mkoani Lindi kama ilivyopangwa.
Tamko hilo lilitolewa na mwenyekiti wa Taso, Engelbert Moyo wakati akizungumza na wajumbe wa kamati ya maandalizi ya sherehe hizo katika kikao kilichofanyika Lindi.
Mwenyekiti huyo alilazimika kukanusha madai hayo kutokana na mjumbe mmoja kuomba uongozi utoe ufafanuzi kuhusu madai yanayoendelea kutolewa na watu kupitia vyombo vya habari.
Mjumbe huyo alisema kuna madai kuwa sherehe hizo zitafanyika mkoa mwingine na si mkoa wa Lindi.
Akijibu hoja ya mjumbe huyo, Moyo alisema kuwa madai hayo yapo huku akiwataka wanaoeneza uvumi kwa lengo la kuupotosha umma kuacha kufanya hivyo mara moja.
Aidha moyo amewataka wananchi kutokubali kuyumbishwa na matamko yanayotolewa na baadhi ya watu,badala yake wajifunge kibwebwe
kuhakikisha Sherehe za maonesho ya nanenane yanafanikiwa ipasavyo.Sherehe za sikukuu za wakulima na maonesho ya Kilimo nanenane,kitaifa mwaka huu, yanafanyika mkoani hapa kwenyeviwanja vya Ngongo ndani yaManispaa ya Lindi.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa