Home » » Waendesha magari tishio kwa utalii

Waendesha magari tishio kwa utalii

Nilishawahi kuandika kuwa tunapozungumzia utalii, mojawapo ya mambo muhimu ni ile ya kuwatembeza maeneo mbalimbali ili kujionea vivutio.
Watalii wamegawanyika katika makundi mbalimbali ikitegemea uwezo wao wa fedha, vitu wanavyohitaji kuviona, na wapi viliko, na pengine kama wanataka kujenga urafiki na jamii wanayoitembelea, kuuliza maswali na kujenga ufahamu zaidi kutoka kwa wenyeji.
Kuna wale ambao wangetaka kutumia fursa ya utalii kupiga picha vivutio au na watu, na kadhalika.
Jambo muhimu kwa utalii ni kuweza kufika mahali kwa urahisi na bila kuwa na hofu ya kuwa na usalama mdogo.
Na hapa sasa kwa watalii waendao au wanaotembea kwa miguu usalama wao barabarani ni muhimu sana, katika hili ni kwamba tunapaswa kudhibiti tabia za waendesha magari. Watalii hawazunguki tu kwa kuangalia ramani, bali kwa kuhakikisha wanapotembea hawapatwi na ajali.
Pia wanahitaji kuheshimiwa kama sehemu ya watumiaji ya barabara. Watalii wanaotoka nchi nyingi zilizoendelea wana utamaduni tofauti kabisa wa matumizi ya barabara.
Waendesha magari wanaheshimu watembea kwa miguu, waendesha magari wanaheshimu taa za barabarani kiasi kwamba hata kama ni usiku wa manane, dereva yuko peke yake barabarani atasimama kwenye taa kama hajaruhusiwa, atapunguza mwendo sehemu wanakopita waenda kwa miguu hata kama hakuna anayevuka.
Atasimama kumpisha mwenda kwa miguu akiona dalili kuwa anataka kuvuka barabara.
Hapa ni vurugu tupu; waendesha magari ndio wenye haki, hawasimami kwenye vivuko vya watembea kwa miguu; wengi wa watembea kwa miguu hulazimika kusimama hadi miguu iwaume wakisubiri kuvuka. Ni kawaida kuona wakipigiwa honi na kutukanwa wakiwa katikati ya barabara, na wapo waliopondwa na kufa. Madereva hawaheshimu taa za barabarani, na wanasahau kwamba wengine pia wana haki ya kutumia barabara.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa