Home » » TPF Net Lindi yatoa Msaada katika kambi ya wazee na walemavu Lindi

TPF Net Lindi yatoa Msaada katika kambi ya wazee na walemavu Lindi

Mwenyekiti wa Mtandao wa Polisi wanawake mkoani Lindi, ambaye pia ni Kamishna msaidizi wa Jeshi hilo,Acp Renatha Mzinga (kulia) akikabidhi sehemu ya msaada wa vyakula kwa Muuguzi wa kambi ya wazee wasiojiweza ya Rasibura,Manispaa ya Lindi,Bi,Elizabeth Njowele.
Kamishna msaidizi wa Jeshi la polisi Mkoani Lindi,Bi. Renatha Mzinga pamoja na wanachama wa mtandao wa Polisi wanawake wakishiriki kazi ya usafi katika kambi ya wazee na walemavu Mkoani Lindi.
Wana mtandao wa Polisi wakiendelea na zoezi la usafi.

Na Abdulaziz Video,Lindi

MTANDAO Wa Polisi Wanawake Mkoani Lindi (TPF-net) Umeipatia kambi ya wazee wasiojiweza msaada wa bidhaa mbalimbali,zikiwemo nguo, vyakula na mafuta wenye thamani ya Sh,309,500/-ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku 16 kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya mwanamke hapa nchini.

Akikabidhi msaada huo,mwenyekiti wa Mtandao huo na Ambae pia ni kamishna msaidizi Polisi mkoani Lindi Acp Renatha Mzinga,alisema wao wakiwa ni wanawake wa jeshi hilo,wameamua kuchanga kidogo walichonacho kutoka sehemu ya posho zao,ili kuwakumbuka wenzao wanaokabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo wazee na walemavu wasiojiweza ikiwa katika kuadhimisha siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili dhidi ya mwanamke, yaliyoanza Novemba 25 na kukamilika Decemba 10.

Acp Mzinga amesema iwapo wazee hao wangekuwa na viungo vyao kamili pamoja na kuwa na maisha mazuri,wasingependa kubaki kuishi katika kambi hiyo,huku wakisubiri kusaidiwa kutoka kwa watu wengine.

“Kama msingekuwa na ulemavu kama mlivyokuwa hivi sasa,msingekuwa na sababu za kuishi katika mazingira ya aina hii hivyo sisi tumeona ni bora tuje tuwafanyie Usafi wa makazi yenu na tuwapatie msaada mdogo uliotokana na michango yetu..alisikika kamanda Mzinga wakati akikabidhi misaada hiyo.

Akipokea msaada huo kwa niaba ya wazee wenzake,mwenyekiti wa kambi hiyo ya wazee,Mohamedi Chitawala,ameushukuru mtandao wa wanawake Jeshi la Polisi mkoani hapa (TPF) kuweza kuwakumbuka watu walio na matatizo mbalimbali yakiwemo ya viungo wanaoishi kwenye kambi hiyo,kwa kuwapatia kile kidogo walichonacho.

Chitawala alisema kitendo cha Mtandao huo kuwasaidia wazee wa kambi hiyo, sio ni furaha bali ni moja ya sehemu utekelezaji wa maagizo ya mwenyezimugu wetu kupitia kwenye vitabu vyake anavyoutaka viumbe vyake walio na uwezo kuwasaidia wenzao wasio na na uwezo wakiwemo wao walemavu.

Katika kambi hiyo,iliyo chini ya kanisa katoriki Jimbo la Lindi,imebaki na wazee walemavu wasiopungua saba (7) wakiwemo wanawake watano na wanaume wawili,kati ya 15 waliokuwepo hapo awali,kufuatia baadhi yao kufariki dunia na wengine kuamua kuondoka kambini hapo,kutokana na kile kinachodaiwa huduma duni wanazozipata katika kambi hiyo.
Chanzo;Michuzi blog

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa