Home » » Wakazi wengi Nachingwea hujisaidia vichakani

Wakazi wengi Nachingwea hujisaidia vichakani



Idadi kubwa ya wananchi  katika wilaya ya Nachingwea Mkoa wa Lindi hawana vyooambapo karibia nusu ya kaya zilizopo wilayani humo wahatumii vyoo bora.

Hayo yalibainishwa na Afisa afya na mazingira wa halmashauri ya wilaya ya Nachingwea,Tumaini Kagina alipokuwa akiwasilisha mada kwenye mafunzo kwa wajumbe wa kamati za afya za vijiji na wahudumu wa afya ya msing.

Amesema kuwa Kati ya kaya 55083 zilizo kwenye wilaya hiyo ni kaya 25112 sawa na asilimia 51 ndio  zenye vyoo vyenye sifa huku wananchi wengi wakijisaidia vichakani na kutaka jitihada za dhati za pamoja ili kufikia lengo la kuhakikisha wananchi wanakuwa na vyoo bora.

Amesema kuwa hali hiyo imeonesha kuwa bado wana safari ndefu ya kufikia lengo ka asilimia 80 ifikapo mwaka 2015 na hivyo amewasihi wananchi kujenga makazi pamoja na vyoo bora.

Alibainisha kuwa kufuatia hali hiyo inaandaliwa kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira ambayo itasisitiza utupaji wa takataka,matumizi ya vyoo bora na kunawa mikono wakati wote na hasa baada ya matumizi ya maliwato ili kusaidia kupunguza hatari ya kupata maradhi ya mlipuko na maradhi mengine.

 Amezitaja sifa za choo bora  kuwa  na pamoja na kuwa na sehemu ya kunawia mikono iliyo na maji safi na ya kutosha katika kibuyu chiriri na sabuni,chenye faragha ya kutosha na kujengwa kwa mali ghafi za kudumu,kisichotoa harufu na kuchafua mazingira,kisicho hifadhi wadudu kama nzi na kinachokubalika na jamii.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa