Home » » Ukata wakwamisha utekelezaji wa miradi Lindi

Ukata wakwamisha utekelezaji wa miradi Lindi

Halmashauri ya manispaa ya Lindi imeshindwa kukusanya ada za leseni za biashara kutokana na kuchelewa kupata mwongozo kutoka serikali kuu na kusababisha kukosa mapato na kushindwa kutekeleza miradi yake katika kipindi cha mwaka 2012/2013.
Hayo yamebainishwa na mkurugenzi wa manispaa ya Lindi Kelvin Makonda katika kikao cha robo ya nne cha baraza la madiwani ambapo amesema kwamba licha ya kukosa ada za leseni lakini pia ilienda sanjari na kukosekana kwa malipo ya mnara wa zantel kutopatikana katika kipindi chote cha mwaka.
 Amesema kuwa changamoto kubwa ilikuwa ni kuchelewa kwa ruzuku kutoka serikali kuu kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyoletwa mwishoni mwa robo ya tatu na kusababisha kuchelewa kuanza utekelezwaji wa miradi ya maendeleo.
Hata hivyo ametaja kuwa mradi wa kilimo cha umwagiliaji Ngongo, mradi wa maji Kineng’ene, mradi wa ujenzi wa mabweni ya wavulana na wasichana sekondari ya  Ng’apa na ujenzi wa madarasa na maabara sekondari ya mingoyo kuwa imekamilika na mingine kufikia hatua za mwishoni.
Pia amesema kuwa watu wapatao 640 wamefanyiwa tathmini mashamba yao na kufanyiwa uthamini wa mali katika kupisha upimaji wa viwanja  katika eneo la Mmongo na Mabano kwa ushirikiano baina ya halmashauri ya manispaa na taasisi ya dhamana ya taifa(UTT).
 Amesema kuwa mradi huo utawezasha manispaa kupata mapato kutokana na mauzo ya viwanja vitakavyouzwa kwa wananchi kwa kugawana na UTT asilimia hamsini ya mapato.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa