Mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi Mhe. Abdalah Ulega wakati wa mahojiano haya
**************************************************************************
Na Abdulaziz Video,Kilwa
MKUU wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi Mhe. Abdalah Ulega ameonya kuwa
hatakuwa na msamaha kwa mzazi yeyote atakayeshindwa kumpeleka mtoto
wake kuanza kidato cha kwanza kwa kisingizio cha umaskini wa kipato.
Akizungumza katika mahojiano na Globu ya Jamii ofisini kwake, Mkuu huyo wa wilaya
amesema kumekuwa na visingizio vingi kutoka miongoni mwa wazazi
wanapohimizwa kuwapeleka watoto wao shule kwa madai kwamba hawana
uwezo.
''Ukiwafuatilia watoto utasikia wazazi wanaanza utetezi Sina
Uniform,Sina ada mara viatu na visababu vingi hii mwandishi siwezi
kuliachia watoto hawa wataishi vipi baadae Wapo wakuu wa
wilaya,madaktari,walimu wa baadae kwa nini tuwasitishie maisha
yao...
"Hii siwezi kukubali na Nimeagiza na si kuagiza tu nitafuatilia
kuhakikisha watoto wanaelimika'
Mkuu huyo wa wilaya amebainisha kuwa endepo katika familia
kutakuwepo na mzazi hasiye jiweza, kinachotakiwa ni kuchukua hatua ya
kumpeleka mtoto wake shuleni kwanza na kwamba mambo mengine yakiwemo
ya ada na sare ya mwanafunzi yataendelea kutekelezwa taratibu wakati
mwanafunzi akiendelea na masomo.
''Sasa Kilwa Inapata mrahaba wa gesi ya songosongo takriban Milioni
100 na hivi karibuni mambo yakienda vizuri Halmashauri itakuwa
inaingiziwa Karibu milioni 300 kutokana na gesi kwa mwezi na Wakubwa
Madiwani wamepitisha kupitia baraza la madiwani kuwa mapato hayo
aslimia 35 iende katika kuboresha elimu
"Je nikiacha raslimali za Kilwa
zitachukuliwa na wageni wenyeji wakiwa watumwa...Kwa hili wazazi
nitaenda nao sambamba na timu yangu ipo imara...Alimalizia Ulega.
Sambamba na hayo ilibainika kuwa hadi
kufikia juma lilopita, jumla ya wanafunzi 414 wakiwemo wavulana 316
wasichana 98 waliochaguliwa kuingia kitado cha kwanza mwaka huu
walikuwa bado hawajaripoti katika shule walizopangiwa
Chanzo Michuzi Blog
0 comments:
Post a Comment