Home » » mkuu wa wilaya ya kilwa aapa kula sahani moja na wazazi wasiopeleke watoto shule

mkuu wa wilaya ya kilwa aapa kula sahani moja na wazazi wasiopeleke watoto shule



Mkuu wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi  Mhe. Abdalah Ulega wakati wa mahojiano haya
 **************************************************************************
Na Abdulaziz Video,Kilwa 
MKUU wa wilaya ya Kilwa mkoani Lindi  Mhe. Abdalah Ulega ameonya kuwa hatakuwa na msamaha kwa mzazi yeyote atakayeshindwa kumpeleka mtoto wake kuanza kidato cha kwanza kwa kisingizio cha umaskini wa kipato. 
Akizungumza katika mahojiano na Globu ya Jamii ofisini kwake, Mkuu huyo wa wilaya amesema kumekuwa na visingizio vingi kutoka miongoni mwa wazazi wanapohimizwa kuwapeleka watoto wao shule kwa madai kwamba hawana uwezo. 
''Ukiwafuatilia watoto utasikia wazazi wanaanza utetezi Sina Uniform,Sina ada mara viatu na visababu vingi hii mwandishi siwezi kuliachia watoto hawa wataishi vipi baadae Wapo wakuu wa wilaya,madaktari,walimu wa baadae kwa nini tuwasitishie maisha yao...
"Hii siwezi kukubali na Nimeagiza na si kuagiza tu nitafuatilia kuhakikisha watoto wanaelimika' Mkuu huyo wa wilaya amebainisha kuwa endepo katika familia kutakuwepo na mzazi hasiye jiweza, kinachotakiwa ni kuchukua hatua ya kumpeleka mtoto wake shuleni kwanza na kwamba mambo mengine yakiwemo ya ada na sare ya mwanafunzi yataendelea kutekelezwa taratibu wakati mwanafunzi akiendelea na masomo.
''Sasa Kilwa Inapata mrahaba wa gesi ya songosongo takriban Milioni 100 na hivi karibuni mambo yakienda vizuri Halmashauri itakuwa inaingiziwa Karibu milioni 300 kutokana na gesi kwa mwezi na Wakubwa Madiwani wamepitisha kupitia baraza la madiwani kuwa mapato hayo aslimia 35 iende katika kuboresha elimu
"Je nikiacha raslimali za Kilwa zitachukuliwa na wageni wenyeji wakiwa watumwa...Kwa hili wazazi nitaenda nao sambamba na timu yangu ipo imara...Alimalizia Ulega.
 Sambamba na hayo ilibainika kuwa hadi kufikia juma lilopita, jumla ya wanafunzi 414 wakiwemo wavulana 316 wasichana 98 waliochaguliwa kuingia kitado cha kwanza mwaka huu walikuwa bado hawajaripoti katika shule walizopangiwa



Chanzo Michuzi Blog

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa