Home » » TMF YAWANOAWANAHABARI NA WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI MKOANI LINDI

TMF YAWANOAWANAHABARI NA WAMILIKI WA VYOMBO VYA HABARI MKOANI LINDI


Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania katika kukuza Uimara Na kujenga Uhuru wa Vyombo vya habari na Waandishi wa Habari unatoa mafunzo kwa kwa Waandishi na wamiliki wa vyombo hivyo Mkoani Lindi ili kuwajengea Uwezo wa kuomba Ruzuku zinazotolewa na Mfuko huo.

Mafunzo hayo ya Siku moja yanawezeshwa na Mshauri wa mambo ya Habari ambae pia ni mwandishi Mkongwe,Bw Ndimara Tegambwage na Meneja wa Vyombo vya Habari vya SJMC Chini ya Chuo kikuu cha DSM,Bi Edda Sanga Kufuatia awamu ya pili ya Utoaji Ruzuku hizo toka TMF,Mfuko umeamua kutoa mafunzo hayo ili kutoa msisitizo katika Uandishi wa Habari za Vijijini,Uwazi na Uwajibikaji,Utawala bora,Ukimwi,Jinsia na kuwapa sauti za jamii zilizotengwa ili waandishi waweze kupata habari kwa jamii na habari zinazogusa jamii.

Katika Mafunzo hayo pamoja na kuwezesha na wakongwe wa habari pia yamehusisha wanahabari na wamiliki toka mkoani humo yanayoweshwa na Afisa Mwandamizi wa TMF,Alex Kanyambo,Afisa Mawasiliano TMF,Japhet Sanga na Bi Raziah Mawanga,,,Afisa Mafunzo Tmf
Picha na Habari..Mdau Abdulaziz video,Lindi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa