WAISLAMU       nchini leo watasherehekea Sikuuu ya Idd el- Fitri ambayo     husheherekewa   mara baada ya kumalizika kwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Tunapenda       kuchukua fursa hii kuwatakia sikukuu njema Waislamu wote nchini na       kuwaomba washerehekee kwa amani na utulivu kama vile walivyokuwa    kwenye    mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Kufunga       mwezi mtukufu wa Ramadhani ni miongoni mwa nguzo tano za Uislamu     hivyo   katika kipindi chote cha funga ya Ramadhani, mbali na kufunga     mchana   anatakiwa azidishe swala mbalimbali na kujiepusha kabisa na     maovu.
Mwezi       mtukufu wa Ramadhani una thamani na historia kubwa kwa Waislamu  kwa      sababu ndio mwezi kiliposhuka kitabu kitakatifu cha Kurani  katika   siku    inayoitwa Lai latul Kadir usiku ambao ni bora kuliko  miezi   1,000.
Si       nia yetu kuanza kuzungumzia kwa undani faida za mwezi wa Ramadhani       lakini katika kipindi chote cha mwezi huu tuliona idadi kubwa ya       Waislamu wakivaa mavazi ya stara, kutenda matendo mema na kualikana       kwenye futari.
Tusingependa       Idd el- Fitri iwe mwanzo wa ajali, maasi, vifo na maovu mengi   ambayo     mara kwa mara tumekuwa tukiyashuhudia kwenye sikuu mbalimbali   hapa     nchini.
Kwa       mujibu wa vitabu vya dini, Mwislamu yeyote akayetenda maovu siku  ya     leo  ni sawa na kufanya dhambi mbele ya Mwenyezi Mungu siku ya   kiama.
Tunaamini       mafunzo waliyoyapata waumini wa Kiislamu kwenye mwezi mtukufu wa       Ramadhani utawasaidia kuishi kulingana na maagizo ya Mwenyezi Mungu  na      kujiepusha na dhambi mbalimbali.
Tunachukua       fursa hii kuwaomba madereva wote wa vyombo vya moto kuchukua     tahadhari   pamoja na kutoendesha kwa kasi wanapovitumia ili kuepusha     ajali   zinazozidi kuongezeka kila kukicha.
Wazazi na walezi wasiwaruhusu watoto wao kwenda matembezini, fukwe za bahari na kumbi za disko bila ya uangalizi maalumu.
Tunasema       hivyo kwakuwa kila mara tumekuwa tukisikia watoto wakipata madhara       kwenye kumbi za disko, kupotea, kuzama baharini na mikasa  mbalimbali      ambayo chanzo chake ni uangalizi mdogo wa wazazi au  walezi.
Kwa       wale wanaokwenda matembezini ni vema wakahakikisha majumbani mwao       kunakuwa salama kwa kumuacha mtu atakayelinda au kuzifunga vizuri  kwa      lengo la kuzuia wezi.
Tunaamini       kuwa Jeshi la Polisi litazidisha ulinzi katika maeneo mbalimbali   ili     kuwadhibiti wale wote waliolenga kufanya uhalifu kwenye sherehe   za  Idd    el- Fitri.
Chanzo: Tanzania Daima
 

 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment