Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof Dos Santos Silayo akiwa kwenye mkutano na watendaji wake wa Kanda ya Kusini (hawapo pichani) muda mfupi kabla ya kuwataka meneja kuchukukua hatua kwa watendaji wasio waadilifu mapema hivi leo.
Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda ya Kusini Ebrantino Mgiye (mwenye koti jeusi) akiwasolisha mafanikio na changamoto zinazoikabili kanda huku akifuatiliwa kwa umakini na Meneja Msaidizi wa Mipango na Matumizi Endelevu ya Rasilimali za Misitu Bw. Gaudence Kilasi (aliyekaa) mapema hivi leo.
Baadhi ya Watendaji wa TFS Kanda ya Kusini wakichukua kumbukumbu katika Kikao cha Wafanyakazi kilichoendeshwa na Mtendaji Mkuu wa TFS Prof Dos Santos Silayo kuanza kuzungumza nao mapema hivi leo hii.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof Dos Santos Silayo akimfuatilia kwa umakini Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda ya Kusini Ebrantino Mgiye (hayupo pichani) alipokuwa akiwasilisha mafanikio na changamoto ya miaka mitatu ya kanda hiyo mapema hivi leo.
Na Tulizo Kilaga Lindi
Mtendaji
 Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Prof Dos Santos 
Silayo amewataka meneja wa misitu nchini kusita kuchukua hatua pale 
wanapokuwa na ushahidi dhidi ya watendaji wanaojihusisha na vitendo vya 
rushwa kwenye vituo vya ukaguzi wa mazao ya misitu.
Ametoa
 agizo hilo leo tarehe 04/10/2017, alipotembelea na kuzungumza na 
wafanyakazi wa TFS Kanda ya Kusini katika ofisi za Wilaya ya Lindi ya 
Taasisi hiyo.
“Kuna
 tuhuma za hovyo nimesikia, watu wanakamatwa na mazao ya misitu 
yaliyovunwa ama kusafirishwa kinyume na sheria, wanaombwa kitu kidogo na
 baadhi ya watumishi wasio waaminifu ili kuhalalisha mizigo hiyo na 
wakigoma, mizigo yao hukamatwa, nataka kuwaona mnachukua hatua 
stahiki,”amesema.
Mtendaji
 Mkuu ameeleza kuwa licha ya TFS kuwa na changamoto nyingi anaimani na 
taasisi hiyo na amewataka watendaji wake kufanya kazi kwa kushirikiana 
na kamati za ulinzi na usalama za mikoa na wilaya na kuzingatia weledi, 
uzalendo na uadilifu, akiahidi Serikali kufanyia kazi changamoto 
zinazowakabili.
Awali,
 Kaimu Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu Kanda ya Kusini Ebrantino 
Mgiye alisema miongoni mwa changamoto zinazokabili taasisi hiyo ni 
pamoja na uhaba wa watendaji.
Hata
 hivyo, Mtendaji Mkuu amewataka watendaji wa TFS kujikita katika 
utendaji wa kimkakati ili kuboresha usimamizi na uhifadhi wa raslimali 
za misitu na Nyuki kwa ajili ya kuchangia katika mahitaji ya kijamii, 
kiuchumi, ki-ikolojia, na ki-utamaduni kwa kizazi cha sasa na kijacho.
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment