Home » » UKINYIMWA UNYUMBA NDANI YA NDOA NENDA KASHITAKI DAWATI LA JINSIA POLISI

UKINYIMWA UNYUMBA NDANI YA NDOA NENDA KASHITAKI DAWATI LA JINSIA POLISI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Na Adili Mhina, Lindi.
Kaimu Katibu Mtendaji, Wizara ya Fedha na Mipango upande wa Tume ya Mipango, Bibi Florence Mwanri amefanya ziara katika eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata Gesi Asilia lililopo katika mtaa wa Likong’o Manispaa ya Lindi na kushauri uongozi wa Manispaa hiyo kuongeza  juhudi za kuhakikisha wananchi waliopisha mradi huo wanalipwa fidia kwa wakati.
Mwanri alieleza kuwa ni vyema uongozi ukatilia mkazo umuhimu wa kuwalipa fidia wananchi ili waweze  kujiletea maendeleo yao kwa kuwa hawawezi tena kuendelea kutumia eneo hilo.
Alieleza kuwa dhamira ya Serikali ya kujenga uchumi wa viwanda inaenda sambamba na kuwajali wananchi wake kwa kutoa fidia kwa mujibu  kanuni na sheria pale wanapolazimika kuachia  maeneo yao ili kupisha miradi ya maendeleo.
Mwanri aliongeza kuwa pamoja na kuwa mradi huo utakapojengwa na kukamilika utakuwa na faida kwa maendeleo ya Taifa kwa ujumla utasaidia pia kuinua kipato kwa wanachi wa Lindi kutokana na fursa mbalimbali za ajira zitakazojitokeza kwa wakazi hao.
 Nae Mtendaji wa Mtaa wa Ling’oko ambapo ndipo mradi huo unapotekelezwa, Bw. Jacob Anton alieleza kuwa wananchi wa eneo hilo wana matarajio makubwa na wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa Serikali kwa kuwa wanaamini ujio wa kiwanda hicho utasaidia kuboresha maisha yao.
Timu ya Ukaguzi wa Miradi kutoka Tume ya Mipango ikiongozwa na Naibu Katibu Mtendaji huyo, kwa sasa inaendelea na zoezi la ukaguzi wa Miradi ya Maendeleo katika Mikoa ya Pwani, Lindi na Mtwara ambapo itatembelea miradi ya Serikali na ile ya sekta binafsi kwa lengo la kuhakikisha malengo ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2016/17-2020/21) yanatekelezwa kwa ufasaha.

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa