Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kushoto Meneja Uhusiano wa Airtel bw Jackson Mmbando akielezea huduma zitakazotolewa na mnara wa Airtel uliojengwa kijiji cha Cheleweni kwa Mkuu wa wilaya Lindi bw, Shaibu Ndemanga (wapili kulia) mara baada ya kuzindua mnara huo huku wananchi wakisikiliza. katikati ni Meneja wa Airtel Lindi by Saleh safy. Airtel imejenga mnara huo kutoa mawasiliano katika vijiji vya Ng’apa ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo yanayowazunguka vijiji hivyo Safy. Airtel imezindua huduma hiyo ili kuboresha , huduma za kifedha kwa njia ya mtandao Airtel Money na kuwaweza wananchi wa Lindi kupata mawasiliano ya uhakika katika kuendesha shughuli zao za kila siku kiuchumi na kijamii
Mkuu wa Wilaya Lindi bw, Shaibu Ndemanga akiongea na wananchi wakati wa uzinduzi wa mnara wa Airtel utakaotoa mawasiiano katika vijiji vya Ng’apa ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo yanayowazunguka vijiji hivyo. anaefuata ni diwani wa viti maalum Lindi Bi, Somoe Pamui na Meneja Mauzo wa Airtek Bw, saleh Safy. Airtel imezindua huduma hiyo ili kuboresha , huduma za kifedha kwa njia ya mtandao Airtel Money na kuwaweza wananchi wa Lindi kupata mawasiliano ya uhakika katika kuendesha shughuli zao za kila siku kiuchumi na kijamii
Mtandao wa Airtel kutumika kuhimiza elimu ili wazazi kuandikisha watoto Lindi vijijini
katika
 juhudu za kuhakikisha huduma za mawasiliano zinawafikia maeneo ya 
pembezoni mwa nchi, kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imezindua 
mnara wake wa mawalisiliano na kuanzisha hduma za simu kwa mara ya 
kwanza katika kijiji cha cheleweni mkoa wa Lindi.
Huduma
 hizi mpya za mawasiliano zitawafikia wakazia wa vijiji vya Ng’apa 
ngapa, Cheleweni, Nchee, Nantumbya, Nanyuru pamoja na maeneo 
yanayowazunguka vijiji hivyo kwa kuwahakikishia wakazi wote wa Lindi 
vijijini huduma za mawasiliano za uhakika, huduma za kifedha kwa njia ya
 mtandao Airtel Money na hatimae kuendesha shughuli zao za kila siku 
kiuchumi na kijamii
Akiongea
 wakati wa uzinduzi, Mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga alisema “ 
tunayofuraha kupata huduma za mawasilino hapa cheleweni na vijiji vya 
jirani.  Airtel kwa kuzindua mnara huu, serikali tunaungano jitiada hizi
 za kuboresha mawasiliano huku vijiji kwa sasa wakazi wa vijiji hivi 
mtaweza kutumia huduma ya mawasiliano kwa kufany a biashara zenu za nazi
 kwa kujitafutia masoko sehemu nyingine lakini pia itasaidia kuondoa 
tatizo lakutembe na fedha nyingi pale mnapofanya biashara kwa kuwa 
mtatumia huduma za kifedha za Airtel Money kujichukulia fedha zenu 
wakati wowote
Mkuu
 wa wilaya aliongeza kwa kusema “Mawasiliano haya yatasaidia sana wilaya
 yangu katika kukuza elimu kwa kuwa nitaweza kuwawasiliana na watendaji 
wangu wote wakati wowote. Sasa nitoe tamko kwamba nimeongea na Airtel 
ili kutuma ujumbe wa meseji kwa wazazi wote kwa kuwa ndio mtandao 
unaotumika na wengi hapa katika vijiji vyetu vya ng’apa ng’apa  kuhusu 
kuandikisha watoto wote waliomaliza shule za msingi waende sekondari, 
 Airtel wamenikubalia sasa ikiwa  mzazi atakaidi kuitikia wito 
nitamchukulia hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kumfunga”.
Nataka
 kuona  huduma hii ya Mtandao wa Airtel tunayoizindua leo inaleta tija 
katika shughuli za uchumi kama vile uzalishaji wa korosho, kusaidia 
biashara ndogo za kati na kubadilisha maisha ya jamii kwa ujumla.  
Napenda kuchukua fursa hii  kuwahasa wakazi pia kuilinda miundombinu ya 
mawasiliano haya ili yaduma. Alimalizia kusema Mh, Ndemanga
Kwa
 upande wake Meneja Mauzo wa Airtel, Saleh Saphy “Tunayofuraha kutoa 
huduma za uhakika na gharama nafuu nchi nzima, kwa wakazi wa Lindi , 
tunawahakikishia ofa kabambe za msimu huu wa sikukuu kupitia ofa yetu 
maalumu ya “Wadatishe” ambayo mnaweza kupata simu orijino kwa gharama 
nafuu hadi ya shilingi 79,000 tu.-. vilevile wateja wanaweza kupata 
vifurushi vya intaneti vya 1G kwa shilingi 1000 wakati huu wa msimu wa 
sikukuu .
Kupitia
 huduma ya mawasiliano wateja wataunganishwa na huduma za intaneti, 
huduma za kifedha za Airtel Money kutuma na kupokea pesa, kupiga simu 
wakati wowote, kusajili simu zao na pia kupata nafasi ya kusoma masomo 
ya ufundi ya VETA kupitia simu zao. Hizi ni baadhi tu za huduma zetu 
hivyo natoa wito kwa wakazi wa cheleweni, Ng’apa na Michee kujiunga na 
timu ya  Airtel SIBANDUKI na kufurahis huduma zetu.” Alisisitiza Saphy
 

 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment