Home » » Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufungua Maonyesho ya Nane Nane Kitaifa mkoani Lindi Agosti 3, mwaka huu

Waziri Mkuu Mizengo Pinda kufungua Maonyesho ya Nane Nane Kitaifa mkoani Lindi Agosti 3, mwaka huu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
01
Lindi kumekucha, pilikapilika za maandalizi ya Maonyesho ya Nane Nane kitaifa mwaka huu zimepamba moto ambapo Mgeni Rasmi katika maonesho hayo yatakayofunguliwa Jumatatu Agosti 3, 2015 anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda. Maonyesho hayo ya mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.
02
03
04
Mratibu wa Maonyesho ya Nane Nane kutoka wilaya ya Newala Ado Kiwangu akiwaonesha na kuwaeleza wageni waliotembelea bustani ya michungwa juu ya namna bora ya kuzalisha machungwa ikiwa ni pamoja na matumizi ya mbolea ya samadi inayoipa michungwa virutubishi stahiki, hivyo michungwa huzaa sana.
05
Mfugaji wa sungura Ahmed Juma Ntava akiwalisha sungura wakati wa maandalizi ya Maonyesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Lindi mwaka huu ambapo Mgeni Rasmi katika maonesho hayo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda yatakayofunguliwa Jumatatu Agosti 3, 2015.
06
Mmoja wa watumishi wa Jeshi la Magereza nchini akivuna kabichi iliyokomaa tayari kwa matumizi ya mboga.
07
Afande Majid Nyange kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) akieleza namna ya kutumia mazingira ya asili kutengeneza jokofu yenye gharama nafuu kwa kutumia mkaa, miti, sakafu na nailoni yeusi kwa ajili ya kusharabu mwanga.
08
09
Maeneo mbalimbali ya bustani na mifugo yaliyoandaliwa tayari kwa maonesho Nane Nane kitaifa mkoani Lindi mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”(Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Lindi).
10
11
12
14
15
16
18
19

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa