Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
      
      
      
       
Lindi
 kumekucha, pilikapilika za maandalizi ya Maonyesho ya Nane Nane kitaifa
 mwaka huu zimepamba moto ambapo Mgeni Rasmi katika maonesho hayo 
yatakayofunguliwa Jumatatu Agosti 3, 2015 anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu 
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda. Maonyesho hayo ya 
mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu “Matokeo Mkubwa Sasa, Tuchague 
Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na Ufugaji”.
Mratibu
 wa Maonyesho ya Nane Nane kutoka wilaya ya Newala Ado Kiwangu 
akiwaonesha na kuwaeleza wageni waliotembelea bustani ya michungwa juu 
ya namna bora ya kuzalisha machungwa ikiwa ni pamoja na matumizi ya 
mbolea ya samadi inayoipa michungwa virutubishi stahiki, hivyo michungwa
 huzaa sana. 
Mfugaji
 wa sungura Ahmed Juma Ntava akiwalisha sungura wakati wa maandalizi ya 
Maonyesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Lindi mwaka huu ambapo Mgeni Rasmi
 katika maonesho hayo anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya 
Muungano wa Tanzania Mizengo Pinda yatakayofunguliwa Jumatatu Agosti 3, 
2015.
Mmoja wa watumishi wa Jeshi la Magereza nchini akivuna kabichi iliyokomaa tayari kwa matumizi ya mboga.
Afande
 Majid Nyange kutoka Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) akieleza namna ya 
kutumia mazingira ya asili kutengeneza jokofu yenye gharama nafuu kwa 
kutumia mkaa, miti, sakafu na nailoni yeusi kwa ajili ya kusharabu 
mwanga.
Maeneo
 mbalimbali ya bustani na mifugo yaliyoandaliwa tayari kwa maonesho Nane
 Nane kitaifa mkoani Lindi mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu “Matokeo 
Mkubwa Sasa, Tuchague Viongozi Bora kwa Maendeleo ya Kilimo na 
Ufugaji”(Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO, Lindi).
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment