Katibu
 Mkuu mstaafu wa Shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi (ICFTU/AFRO), 
Andrew Kailembo(kulia), akiwa katika mkutano wa wadau mbalimbali wa 
kujadili maendeleo ya mkoa wa Kagera uliofanyika jana.
 Wakili wa Kujitegemea, wa IMMMA ADVOCATES, Protas Ishengoma akiongoza mkutano huo.
 REV.Fr
 Kamugisha (kulia), ambaye ni Mkurugenzi wa Hoteli ya Kolping akichangia
 mada. Kutoka kushoto ni Mshauri wa Kimataifa wa Kujitegemea, Fr, James 
Rugemalira na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Kanali mstaafu, Fabian Masawe.
 Wanahabari wa mkoa wa Kagera wakiwa kwenye mkutano huo.
Mkuu
 wa Utawala wa Jumuia ya Afrika Mashariki, mstaafu, Abdul Katabaro naye 
alipata fursa ya kuchangia katika mkutano huo muhimu wa kuhimiza 
uwekezaji mkoani humo.
MSHAURI wa
 Kimataifa wa kujitegemea (International Independent Consultant) Fr. 
James Rugemalira, wa Mabibo Breweries, jana aliandaa hafla ya 
kuzungumzia fursa za maendeleo katika mkoa wa Kagera ndani ya mtangamano
 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 
Hafla hiyo ilihudhiriwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali  Mstaafu Fabian Massawe, ambaye alikuwa Mgeni Rasmi. 
Wengine
 waliohudhuria ni pamoja na wana Kagera wanaoishi na kufanya Kazi nje ya
 mkoa wa Kagera wakiwemo wakili wa kujitegemea Bw. Protase Ishengoma wa 
IMMMA Advocates, mfanyabiashara na Mshauri wa Fr. James, Bw. Abdul 
Katabaro ambaye amestaafu kutoka utumishi wa Jumuiya ya Afrika 
Mashariki, Mzee Andrew Kailembo kutoka Bruxelles, Rev. Fr. David na 
Kyabukoba, miongoni mwa wengi. 
Hafla
 hiyo iliyofanyika kwenye hoteli ya Kolping, mjini Bukoba, pia 
ilihudhiriwa na waandishi wa habari kutoka kwenye vyombo mbalimbali vya 
habari.
Fr.
 James alisisitiza juu ya mkoa kuzitumia fursa nyingi za uchumi 
zinazotokana na jiografia ya mkoa wa Kagera kupakana na nchi zote za 
Jumuiya ya Afrika Mashariki, zikiwemo Burundi, Rwanda, Uganda na Kenya 
kwa maana hiyo kuufanya mkoa huo kuwa ndicho kiunganishi cha nchi zote 
(hub). 
Kwa
 sababu hiyo alisisitiza umuhimu wa mkoa wa Kagera kuwa na miradi 
mikubwa ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa uwanja wa Ki-mataifa 
Omukajunguti, ujenzi wa Bandari Kavu na maeneo huru ya Uzalishaji (EPZ) 
eneo la Kitengule na kilimo cha Matunda, mboga na mazao mengine ya 
chakula. Alisisitiza kuwa soko la mazao lipo katika nchi zinazouzunguka 
mkoa wa Kagera.
Fr.
 James aliitumia fursa hiyo kuelezea mipango ya kampuni ya Mabibo 
Breweries kuwekeza kwenye kiwanda cha kuzalisha bia aina ya Windhoek 
katika mikoa ya Kagera, Tanga na Kilimanjaro. 
Pia
 alizungumzia mpango wa kuanzisha taasisi ya ki mataifa ya uchunguzi na 
tiba kwa maradhi ya Kansa kitakachojulikana kama RUTAKWA BYERA 
INTERNATIONAL DREAM TANK CANCER CENTER ndani ya Manispaa ya Bukoba.
Naye
 Mkuu wa Mkoa alimshukuru sana Fr. James kwa moyo wa uzalendo wa 
kuhamasisha uwekezaji katika mkoa wa Kagera na yeye mwenyewe na Mabibo 
Breweries kuwa msitari wa mbele kwa vitendo. Kanali Massawe 
alimuhakikishia kwamba Serikali ya Mkoa itampatia yeye pamoja na 
wawekezaji wengine watakaojitokeza, ushirikiano wa dhati ili kuhakikisha
 uchumi wa mkoa unapanuka na kuongeza ajira kwa vijana.
Kanali
 Massawe aliwaambia washiriki wa hafla hiyo kuwa alipofika kwenye mkoa 
wa Kagera miaka saba iliyopita, mkoa ulikuwa unashika nafasi ya tatu 
kutoka mwisho kati ya mikoa 25 katika uchumi lakini sasa mabadiliko 
makubwa yamekuwepo mkoa upo kwenye nafasi ya kumi na Sita. 
Aliongeza
 kusema kwamba kwa fursa zilizopo, endapo zitatumiwa vizuri, basi mkoa 
unaweza kufanya vizuri zaidi. Kanali Massawe, aliziainisha fursa nyingi 
zilizopo na ambazo hazijasisimiliwa kuwa ni pamoja na Utalii ambao mkoa 
unavyo vivutio vingi ikiwa ni pamoja na Ziwa Victoria, mto Kagera, watu 
na Utamaduni wao, historia, kituo cha hija cha Nyakijoga na Makanisa 
makubwa yaliyojengwa zaidi ya miaka mia moja iliyopita.
Waalikwa
 mbalimbali waliopata fursa ya kuongea walimpongeza sana Fr. James kwa 
jitihada zake na kuwahamasisha /kuwashirikisha wengine katika kusukuma 
gurudumu la maendeleo ya mkoa wa Kagera.
 Naye
 mwakilishi wa waandishi wa habari waliohudhuria, aliahidi kwamba 
watatoa ushirikiano mkubwa wa kuihabarisha jamii kwa ufasaha juu ya 
jitihada zote za kusukuma mbele gurudumu la maendeleo
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment