HALMASHAURI
 ya Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, imeingia mkataba na nchi za Ulaya, 
ikiwemo Serikali ya Ufaransa wa kusimamia, kutunza na kuendeleza 
rasilimali za urithi yakiwemo mambo ya kale yaliyopo katika wilaya hiyo.
Zoezi
 la kutiliana saini juu ya mkataba huo, ulioongozwa na Balozi wa nchi 
hizo ,Filberto Sebregodi, limefanyika Ukumbi wa Jengo la PEC uliopo mji 
mdogo wa Masoko. 
Hayo yameelezwa na Balozi wa wanchi hizo za umoja 
wa Ulaya Filiberto Sebregodi, alipokuwa akizungumza katika mkutano 
uliowakutanisha wadau wa masuala ya utalii wilayani Kilwa. 
Mkataba 
huo wa miaka mitatu, una lengo la kuendeleza masuala ya mambo ya kale 
(Utalii) unahusisha masuala ya usimamizi na utunzaji wa mambo ya Kale, 
yakiwemo magofu misikiti na nyumba zilizopo visiwa vya Songo Mnara na 
Kilwa kisiwani. 
Akizungumza kabla ya kutiliana saini kwa mkataba huo
 ,Balozi wa Nchi za Umoja wa Ulaya, Filiberto Sebregondi, alisema nchi 
hizo zimeamua kushirikiana na Halmashauri hiyo, kutangaza rasilimali za 
Urithi zilizopo katika wilaya hiyo, ili kukuza maendeleo ya kiuchumi na 
kijamii ndani ya wilaya hiyo.
Balozi huyo amesema Kilwa ni wilaya 
iliyo na vivutio vya kila aina vya utalii, ambavyo kama vitatunzwa na 
kutangazwa vitaweza kukuza utalii wake wa ndani na kuongeza uchumi kwa 
wananchi wake na serikali kwa ujumla. 
Alisema kufuatia kuwepo kwa 
vivutio hivyo, ndipo Ubalozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya na Serikali ya 
Ufaransa ikaamua kusaini mkataba wa miaka mitatu na Halmashauri ya 
wilaya hiyo ya Kilwa katika kutunza, kusimamia na kuendeleza rasilimali 
za urithi zilizopo wilayani.
" Kilwa ni wilaya tajiri kwani ina 
rasilimali nzuri tu, hususan zile zakiutalii, lakini hazifahamiki 
kutokana na kutotangazwa,"alisema Balozi Filiberto Sebregodi. 
Naye, 
mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Mohamedi Ally Mtopa, 
akitoa shukrani zake kwa niaba ya wananchi wa wilaya, ameishukuru nchi 
za Ulaya kwa kutupatia mradi huo, kwani utaendelea kuimarisha rasilimali
 za mambo ya kale.
Mtopa akasema bado Kilwa itaendelea kudumisha 
uhusiano wa kirafiki kati yake na nchi hizo za Ulaya ikiwemo ya 
Ufaransa, kwani yapo mambo mengi wanayoyahitaji kutoka katika nchi hizo.
 
Mradi huo wa miaka mitatu na utaenda sanjari na kubadilishana 
uzoefu kwa sababu rasilimali za urithi zilizopo Ufaransa ambazo 
zinawaingizia fedha na kukuza uchumi kwa wananchi wa wilaya hiyo ya 
Kilwa
Chanzo;Majina 
 
0 comments:
Post a Comment