Home » » Kilwa waingia mkataba na Ulaya kutunza rasilimali

Kilwa waingia mkataba na Ulaya kutunza rasilimali

HALMASHAURI ya Wilaya ya Kilwa mkoani Lindi, imeingia mkataba na nchi za Ulaya, ikiwemo Serikali ya Ufaransa wa kusimamia, kutunza na kuendeleza rasilimali za urithi yakiwemo mambo ya kale yaliyopo katika wilaya hiyo.

Zoezi la kutiliana saini juu ya mkataba huo, ulioongozwa na Balozi wa nchi hizo ,Filberto Sebregodi, limefanyika Ukumbi wa Jengo la PEC uliopo mji mdogo wa Masoko.
Hayo yameelezwa na Balozi wa wanchi hizo za umoja wa Ulaya Filiberto Sebregodi, alipokuwa akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wadau wa masuala ya utalii wilayani Kilwa.
Mkataba huo wa miaka mitatu, una lengo la kuendeleza masuala ya mambo ya kale (Utalii) unahusisha masuala ya usimamizi na utunzaji wa mambo ya Kale, yakiwemo magofu misikiti na nyumba zilizopo visiwa vya Songo Mnara na Kilwa kisiwani.
Akizungumza kabla ya kutiliana saini kwa mkataba huo ,Balozi wa Nchi za Umoja wa Ulaya, Filiberto Sebregondi, alisema nchi hizo zimeamua kushirikiana na Halmashauri hiyo, kutangaza rasilimali za Urithi zilizopo katika wilaya hiyo, ili kukuza maendeleo ya kiuchumi na kijamii ndani ya wilaya hiyo.
Balozi huyo amesema Kilwa ni wilaya iliyo na vivutio vya kila aina vya utalii, ambavyo kama vitatunzwa na kutangazwa vitaweza kukuza utalii wake wa ndani na kuongeza uchumi kwa wananchi wake na serikali kwa ujumla.
Alisema kufuatia kuwepo kwa vivutio hivyo, ndipo Ubalozi wa Umoja wa Nchi za Ulaya na Serikali ya Ufaransa ikaamua kusaini mkataba wa miaka mitatu na Halmashauri ya wilaya hiyo ya Kilwa katika kutunza, kusimamia na kuendeleza rasilimali za urithi zilizopo wilayani.
" Kilwa ni wilaya tajiri kwani ina rasilimali nzuri tu, hususan zile zakiutalii, lakini hazifahamiki kutokana na kutotangazwa,"alisema Balozi Filiberto Sebregodi.
Naye, mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa, Mohamedi Ally Mtopa, akitoa shukrani zake kwa niaba ya wananchi wa wilaya, ameishukuru nchi za Ulaya kwa kutupatia mradi huo, kwani utaendelea kuimarisha rasilimali za mambo ya kale.
Mtopa akasema bado Kilwa itaendelea kudumisha uhusiano wa kirafiki kati yake na nchi hizo za Ulaya ikiwemo ya Ufaransa, kwani yapo mambo mengi wanayoyahitaji kutoka katika nchi hizo.
Mradi huo wa miaka mitatu na utaenda sanjari na kubadilishana uzoefu kwa sababu rasilimali za urithi zilizopo Ufaransa ambazo zinawaingizia fedha na kukuza uchumi kwa wananchi wa wilaya hiyo ya Kilwa

Chanzo;Majina

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa