Home » » KICHANGA CHAOKOLEWA NDANI YA SHIMO LA CHOO

KICHANGA CHAOKOLEWA NDANI YA SHIMO LA CHOO

Nachingwea. Mtoto mchanga mwenye umri wa siku mbili amenusurika kufa baada ya mama yake mzazi, Hadija Pangani (29) Mkazi wa Kijiji cha Mpiruka Wilaya Nachingwea, Lindi kumfunga kwenye kiroba na kumtumbukiza chooni.
Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Mpiruka, Simon Rashidi alisema mtoto huyo aligunduliwa na Techla Sameul baada ya kusikia sauti ya kulia alipokuwa anajisaidi kwenye choo hicho.
Simon alisema baada ya kusikia kelele za mtoto huyo, Techla alitoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya kijiji hicho, ambao kwa pamoja na kushirikiana na jamii na kufanikiwa kumwokoa mtoto huyo ambaye alikutwa hai akiwa amezungushiwa gagulo na kufungwa kwenye kiroba.
Rashidi alisema wakazi wa eneo wakishirikiana na uongozi wa kijiji walifanya uchunguzi na kubaini kuwa mtoto huyo alikuwa wa Hadija kwa kuwa alikuwa na ujauzito kwa kipindi hicho. “Tulimfuata na baada ya kumbana kwa maswali, alikiri kufanya unyama huo kwa madai kuwa ameelemewa na familia, kwani tayari ana watoto watatu kila mmoja na baba yake na hakuna hata mmoja anayetoa masaada.
Kamanda wa Polisi Lindi, George Mwakajinga alithibitisha kutokea ka tukio na kwamba mtuhumiwa atafikisha mahakamani.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa