Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mkuu
 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Michael Isamuhyo akipata
 maelezo kutoka  Mtaalam wa Kutathimini mafunzo  wa VETA  Joyce Mwinuka 
 juu ya VETA inavyofanya kazi katika kuwajenga vijana katika mafunzo ya 
elimu ya ufundi stadi katika maonesho ya Nanenane katika viwanja vya 
Ngongo mkoani Lindi.
 Mkuu
 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Michael Isamuhyo akipata
 maelezo kutoka kwa Meneja uhusiano wa VETA, Sitta Peter wakati mkuu wa 
JKT alipotembelea maonesho ya Nanenane katika viwanja vya Ngongo mkoani 
Lindi.
 Mkuu
 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Michael Isamuhyo akipata
 maelezo wa tofari ambazo zinaokoa gharama kutokana mazingira ambayo 
kila mwananchi anaweza kumudu wakati mkuu wa JKT alipotembelea maonesho 
ya Nanenane katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Shamba darasa la JKT ndani maonesho ya Nanenane katika viwanja vya Ngongo mkoani Lindi.
Na Chalila Kibuda, Lindi.
Mkuu
 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Michael Isamuhyo 
ameiomba Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) kubuni 
mpango maalum wa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana wanaoingia katika 
mafunzo ya JKT ili wakitoka katika makambi waweze kupata fursa za ajira 
katika maeneo mbalimbali.
Meja
 Isamuhyo alitoa ombi hilo Jumatatu, Agosti 7, 2017 alipotembelea kwenye
 banda la VETA, katika maonesho ya Nanenane yanayofanyika kitaifa kwenye
 uwanja wa Ngongo, mkoani Lindi.
Alisema
 vijana wanapoingia katika makambi ya JKT hupata mafunzo ya uzalendo na 
ukakamavu kwa kipindi cha takribani miezi mitatu na kisha kuingia katika
  mafunzo ya stadi za maisha na stadi za kazi kwa kipindi kipatacho 
miezi 18.
Alifafanua
 kutokana na mgawanyiko huo wa mafunzo ya JKT, VETA kwa kushirikiana na 
jeshi hilo wanaweza kuweka mpango maalum wa kutumia kipindi cha miezi 18
 ya mafunzo ya stadi za kazi na stadi za maisha kuandaa mafunzo ya 
ufundi stadi ili kuwapatia vijana ujuzi utakaowawezesha kuajirika baada 
ya kuhitimu JKT.
Alisema
 JKT wamekuwa wakitoa mafunzo ya ufundi stadi mbalimbali, lakini 
changamoto imekuwa ni kukidhi vigezo vya kutunuku vyeti vinavyotambulika
 na VETA, kwani kipindi cha miezi minane ni kifupi katika kukidhi 
matakwa ya mitaala ya VETA.
Alisema
 kutokana na vijana hao kushindwa kupata vyeti vinavyotambulika na VETA 
ambayo ni mamlaka ya kitaifa inayodhibiti na kusimamia mafunzo ya ufundi
 stadi, inakuwa vigumu kwao kukubalika katika ajira au kujiendeleza 
katika maeneo mbalimbali ya stadi walizozipata.
Alishauri
 kuwa, kama mazungumzo na mipango mizuri itawekwa na VETA kwa 
ushirikiano na JKT, kipindi hicho cha miezi 18 ya mafunzo ya JKT 
kinaweza kupangwa vyema katika namna ambayo vijana watatimiza masaa 
yanayohitajika kufuzu mafunzo ya ufundi stadi katika ngazi husika, hivyo
 kutunukiwa vyeti vinavyotambulika na VETA.
Akijibu
 juu ya suala hilo, Meneja Uhusiano wa VETA, Sitta Peter alimshukuru 
Mkuu wa JKT huyo kwa ushauri na mawazo mazuri na kuahidi kuyafikisha 
katika Menejimenti ya VETA kwa majadiliano na utekelezaji.
Alikiri
 kuwa ni kweli kundi hilo la vijana wanaoingia katika mafunzo ya JKT ni 
nguvukazi muhimu ikiwa wataandaliwa vyema katika mafunzo ya ufundi stadi
 baada ya mafunzo ya ukakamavu na uzalendo yanayotolewa na JKT.
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment