Home » » KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI TIGO YATOA OFA KABAMBEYA SIMU ZA KISASA MAONESHO YA NANE NANE -LINDI

KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI TIGO YATOA OFA KABAMBEYA SIMU ZA KISASA MAONESHO YA NANE NANE -LINDI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Meneja Mauzo Kampuni ya Tigo Mkoa wa Mtwara, Lilian Mwalongo akionesha simu mpya ya Tecno R6 kwa baadhi ya wananchii waliofika katika banda la Tigo katika maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea Mkoa wa Lindi.
.Moja ya kikundi cha Timu ya  Mauzo Tigo wakiwa katika picha ya pamoja katika maonesho ya Kilimo yanayoendelea Mkoani Lindi.



Meneja Mauzo Kampuni ya Tigo Mkoa wa Mtwara, Lilian Mwalongo akionesha simu mpya ya Tecno R6 kwa baadhi ya wananchii waliofika katika banda la Tigo katika maonesho ya Kilimo ya Nane Nane yanayoendelea Mkoa wa Lindi.

·         Wakati maadhimisho haya yanafanyika mkoani Lindi kitaifa, Tigo inashiriki kikamilifu katika maadhimisho ya Nanenane katika mikoa ya MorogoroMbeya, Dodoma, Arusha, Mwanza na Tabora.
·         Pia kama ilivyo kawaida yetu ya kuwajali wateja na wananchi kwa ujumla kupitia bidhaa na Huduma zetu bora, kupitia msimu huu wa Nanenane tunatoa ofa kabambe kuhakikisha wananchi wanaendelea kufurahia maisha ya kidigitali. Ofa hizi ni kwa simu za kijanja aina ya Tecno S1 kwa bei ya TZS 99,000/- na Tecno R6 kwa bei ya TZS 195,000 tu. Unaponunua simu hizi unapata mpaka GB 3 za kuperuzi na mtandao ulioboreshwa zaidi Tanzania. 
·         Hii ni sababu tosha kwa wakazi wote wa Lindi na mikoa mingine ambapo maonyesho haya ya Nanenane yanaendelea kuwahi katika banda la Tigo na kujinyakulia simu ili kupata nafasi ya kujishindis Zawadi tulizozitaja.

 Hayo yalisemwa na Meneja Mauzo wa Tigo mkoa wa Mtwara, Lilian Mwalongo kwenye maonesho hayo jana


0 comments:

 
Supported by Tone multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Lindi Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa